SAMATTA ACHAGULIWA MCHEZAJI BORA TP MAZEMBE

Mshambuliaji wa Taifa Stars, Mbwana Samatta amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mwaka na mashabiki wa klabu yake ya TP Mazembe katika ya mchezaji bora wa mwaka wa klabu hiyo iliyopewa jina la"Corbeau d'Or".

Samatta ambaye amepewa jina la utani la"Samagoal"na mashabiki wa TP Mazembe aliwabwaga wachezaji wengine watano waliokuwa wakishindana.

Baada ya zoezi zima la upigaji kura matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:

1. Mbwana Samatta–Kura 248

2. Asante Solomon–Kura 219

3. Robert Kidiaba–Kura 200

4. Nathan Sinkala–Kura 97

5. Rainford Kadaba–Kura 67.