JWTZ KUWACHUNGUZA MAKOMANDO WA NEPAL

JESHI la Wananchi Tanzania(JWTZ), limeshtushwana taarifa za kuwepo kwa makomandoo wa kijeshi kutoka nchi ya Nepal ambao waliingia nchini kinyemela kwa madai ya kutafuta kazi.

Pia, JWTZ imesema taratibu za mwanajeshi kwenda kuajiriwa sehemu nyingine ya nchi haipo karibu duniani kote, hivyo suala hilo wanalifuatilia kwa karibuili kupata undani wake, ambapo hati za kusafiria za makomandoo hao zikiwa zinashikiliwa, huku Serikali ikibeba jukumu la kuwahudumia.

Akizungumza na gazetihili jana kwa njia ya simu,Mkurungenzi wa Idara ya Mawasiliano JWTZ, Luteni Kanali Erick Komba alisema kwa mujibu wa kanuni za jeshini kwamba, mwanajeshi kutoka nchi moja kwenda nyingine suala halipo.

Hata hivyo, Komba alisema inawezekana kukawa na makubaliano maalumu ya nchi au katika jumuia za kusaidia kijeshi, ndipo wanajeshi waliokubalika nchi na nchi hutolewa kwa lengo la kazi maalumu, kama ilivyo kwa vikosi vya kulinda amani ambavyo JWTZ hushiriki.

"Wanajeshi kwa kawaida haajiriwi kama wafanyakazi wengine, ila huteuliwa na jopo maalumu na baada ya kuridhishwa, hupewa nafasi ya kujiunga na jeshi, hivyoni mapema kulisemea na ningeomba uwasiliane na watu wa uhamiaji kwa maelezo zaidi,"alisema Luteni Kanali Komba.

Mkuu wa Idara ya Uhamiaji Dar es Salaam, Grace Hokororo alisema tayari wahamiaji 12 wa Nepal wametumiwa tiketi kutoka kwa ndugu zao na wanatarajiwa kusafirishwa kurejea kwao Septemba 2, mwaka huu.

Alisema wanawashikilia wahamiaji 50, ambapo 12 kati yao ndiyo walioletewa tiketi na waliobaki wanaendelea kuhifadhiwa kama walivyokutwa kwenye nyumba ya mzee mmoja ambaye hakumtaja jina lake.

"Tumefi kia hatua ya kumwomba mzee atusaidie kuwatunza kwenye nyumba hiyo walimokamatiwa, wakati taratibu nyingine zikifanyika, ikiwa pamoja na kuwatafut amawakala wawili waliowaleta nchini," alisema.

Hokororo alisema mawakala waliowaleta wahamiaji hao,walifahamika kwa majina ya Ali Hamidu Ali au kwa jina lingine anajulikana kama Ali Prosper Ngurigwa ambaye ni Mtanzania akishirikiana na raia wa Nepal, Devi Ram Dhamala akiwa na pasipoti 4277471.

Alisema kwa mujibu wataarifa zilizopatikana kutoka kwa wahamiaji hao, zinasema waliletwa nchini baada ya kurubuniwa kuwa, kuna kazi zenye ujira mzuri watakazo pata pindi wakifika Tanzania."

Kuna gharama walilipa, pia kulipa tiketi ya kwenda na kurudi, lakini cha ajabu walipofi kahapa nchini kupitia uwanja wandege, walipelekwa Kijitonyama na Tegeta kwa mafungu na kula yao ikawa ya shida hadi suala hilo lilipofahamika hadharani.

"Hatuwezi kuwaweka ndani kutokana na sheria zilizopo za ndani na nje ya nchi, kwa vile watu hao walidaganywa kwa lengo la kupata ajira, hivyo wanakuwa waathirika wa janga hilo," alisema na kuongeza kwa sasa Serikali imechukua hatua ya kuwahudumia hadi watakapo ondoka nchini.

Makomandoo hao walikamatwa juzi maeneo ya Tegeta jijini Dar es Salaam wakiwa wamehifadhiwa katika nyumba mbili tofauti, huku wakiwa na sare za kijeshi la Nepal.

Chanzo: Jambo Leo