WATU NANE WAFARIKI KATIKA AJALI

Watu nane wamefariki dunia na tisa kujeruhiwa baada ya gari mali ya mfuko wa hifadhi ya jamii TASAF wilaya ya Masasi kumkwepa mbuzi na kuacha njia na kuua watu nane waliokuwa wamekaa pembezoni mwa barabara kuu ya Lindi Mtwara.

Akizungumza kamanda wa polisi mkoa wa Lindi Tenatha Mzinga amethibitisha kufariki kwa watu hao ambapo saba walikufa papo hapo na mmoja amefariki asubui ya leo katika hospitali ya Nyangawa iliyopo jimbo la mtama wilaya ya Lindi vijijini.

Akizungumzia mazingira ya ajali kamanda Mzinga amesema imesababishwa na mwendo kasi wa dereva aliyefahamika kwa jina la Kesi Mwaijande ambapo amesema baada ya kumwepa mbuzi alikosa mwelekeo na kuwazoa.

Kwa upande wake daktari wa zamu Manfid Nyangali amethibitisha kupokea maiti zaba na majeruhi.

Wakizungumzia ajali hiyo wananchi wa kijiji cha Mtama jimbo la Mtama wanahaya ya kusema gari hiyo yenye namba za usajili STl 1615 Landrover iliyokuwa imebeba madiwani sita wa halmashauri ya mji wa Masasi ilikuwa ikitokea kwenye kilele cha maonyesho ya nanenane mkoani Lindi.