WATUPWA SIKU 1 JELA KWA KUKOJOA HADHARANI

Watu 109 wamehukumiwa kifungo cha siku moja jela kwa kukojoa hadharani huko India.

Polisi waliwakamata takriban watu 109 kwa kukojoa katika vituo vya usafiri wa umma na reli.

Wale wote waliokamatwa wanatuhumiwa kwa kupatikana na hatia ya kukojoa nje ama ndani ya vituo vya reli mjini Agra Kaskazini mwa India.

Waliokamatwa watahukumiwa kifungo cha saa 24 korokoroni ama walipe faini ya kati ya dola mbili na kumi au vyote.

Maafisa wa afya ya umma wanasema walifanya operesheni hiyo kwa ghafla ilikukabili uvundowa mkojo unaoathiri afya ya mamilioni ya watu wanaotumia huduma hiyo ya reli nchini India.

Mkuu wa polisi katika eneo hilo GRP, Gopeshnath Khanna aliyeongoza operesheni hiyo anasema kuwa itaendelea hadi wahindi wanaolaumiwa kwa kuharibu mazingira kwa kutema mate ukutani baada ya kutafuna thambuu na tumbako iliyowekwa rangi na kukojoa katika maeneo ya umma watakapo badili tabia zao.

Aidha wasafiri wa reli wanasemekana kupigwa na harafu mbaya ya mkojo pindi wanapoingia ndani ya vituo hivyo.

Operesheni hiyo ni sehemu ya kampeini ya waziri mkuu mpya wa India Narendra Modi ya kuimarisha afya ya umma al maarufu 'Swachh Bharat.

Waandishi wa habari katika eneo hilo la Agra wanasema hii ndio mara ya kwanza kwa maafisa wa kulinda afya ya umma kwa ushirikiano na serikali ya majimbo kuwakamata vikojozi.

Takwimu za afya nchini humo zinaonesha kuwa takriban watu milioni mia sita 600 m ama nusu ya raia wa India hawana vyoo.

WATU WATATU WAFARIKI WAWILI KATI YAO WAHISIWA KUWA MAGAIDI

Watu watatu wamefariki dunia wawili kati yao wanasaidikiwa kuwa ni kundi la magaidi pamoja na raia mmoja baada mapigano kutokea kufuatia msako uliofanywa na jeshi la polisi kwa kundi la vijana wanaojinadi kuwa ni magaidi wapato 50 waliokuwa na silaha mpakani mwa mkoa wa Tanga na Morogoro kupitia msitu wa mziha turiani wilayani Mvomero.

Kamishina msaidizi wa jeshi la polisi mkoa wa Morogoro(ACP) Mussa Marambo akizungumza na waandishi wa habari ofisi kwake amesema jeshi la polisi mkoa wa Morogoro wakishirikiana na askari wa mkoa wa Tanga linawashikilia watu sita wanaojinadi kuwakundi la magaidi kufutia msako mkali uliofanyika baada kuona kundi la vijana wasiojulikana watokako wakiwa na silaha mbalimbali za moto wakielekea mkoani morogoro na wamekimbilia katika misitu.

Kwamujibu wa matroni wa zamu katika hospital ya Bwagala Turiani Lidya mhina akizungumza amethibitisha hospitali imepokea maiti mbili ambazo si raia wa Tanzania pamoja na majeruhi mmoja raia ambaye alifariki muda mfupi wakati akipatiwa matibau na askari mmoja aliejeruhiwa amelazwa anaendelea kwa matibabu katika hospitali hiyo.

KONDOM ZINAZOTAMBUA MAAMBUKIZI YA ZINAA

Wanafunzi katika shule moja nchini Uingereza wameunda mipira ya kondomu inayowaonya watumiaji wanapojamiana na mtu aliyeambukizwa maradhi ya zinaa.

Kondomu hiyo inabadili rangi pindi inapokutana na majimaji ya mtu anayeugua maradhi ya zinaa.

Kondomu hiyo S.T.EYE inaweza kutambua maambukizi ya Chlamydia Kaswende na Kisonono.

Kulingana na wanafunzi hao kondomu hiyo inabadili rangi tofauti kulingana na bakteria iliyopo.

Uvumbuzi huu ni wa Daanyaal Ali, 14, Muaz Nawaz, 13 na ChiragShah, 14, ambao ni wanafunzi katika shule ya Isaac Newton Academy iliyoko Ilford, Essex, nchini Uingereza.

''Tuliazimia kumpa onyo mtumiajiwa mipira hii kuwa mpenzi wake yuko salama ama ni mgonjwa bilaya wasiwasi wa kupimwa hospitalini''.

Wanafunzi hao tayari wametunukiwa, tuzo la ubunifu la''the TeenTech''.

Daanyall alisema kuwa"Walizindua kondomu hiyo ilikuifaidi kizazi kijacho''

''Kwa hakika swala la usalama wa mpenzi wako ni swala la kibinafsi kwa hivyo ni swala linalopaswa kupewa kipaombele haswa ikifahamika kuwa tunawajibu wa kuchochea ngono salama bila ya kuwashurutisha wapenzi wetu kufika hospitalini bila wao wenyewe kukusudia''

Wanafunzi hao waliwalitunukiwa pauni elfu moja pamoja na fursa ya kuzuru Kasri la Malkia wa Uingereza Buckingham Palace.

Muasisi wa kampuni ya ubunifu wa kiteknolojia, TeenTech, Bwana Maggie Philbin, alisema kuwa

"Ni wajibu wetu kama jamii kuchochea ubunifu unaopatikana madarasani kuchochewa na kupigwa msasa kwa minajili ya kuboresha maisha ya mwanadamu''

MWANAMKE MTANZANIA AKAMATWA NA KILO 74 ZA UNGA

Matukio ya Watanzania kukamatwa nje ya nchi wakiwa na dawa za kulevya zilizopigwa marufuku yanazidi kukithiri baada ya mwanamke mmoja kukamatwa na kilo 74 zadawa aina ya ephedrine kwenye Uwanja wa Ndege wa Mumbai, India.

Mwanamke huyo, Chambo Fatuma Basil alikamatwa na Kikosi cha Kupambana na Dawa za Kulevya cha India kilichopata taarifa za kuwapo kwa mtu huyoambaye alikutwa na hati ya kusafiria ya Tanzania.

Kwa mujibu wa tovuti ya hindustantimes.com limewanukuu maofisa wa Idara ya Uhamiaji wa India, Kitengo cha Intelijensia cha Uwanja wa Ndege (AIU) wakisema Chambo alithibitishwa Mtanzania baada ya kufanyia ukaguzi na kukibainisha kuwa kiwango alichokutwa nacho ni kikubwa kulivyo mzigo wowote wa dawa za kulevya uliowahi kukamatwa kwenye uwanja huo wa ndege.

Maofisa hao walisema walimnasa mwanamke huyo baada ya kudokezwa na kufuatilia taarifa ya abiri huyo aliyekuwa akielekea Dar es Salaam kupitia Doha, Qatar.

"Mtuhumiwa alikamatwa saa 7:00 mchana. Mbwa maalum alielekezwa kukagua mizigo yake iliyokuwa inaingizwa chini ya ndege na akatoa ishara chanya," alisema Milind Lanjewar, kamishna wa ziada waushuru wa Uwanja wa Ndege.

Mizigo yake mitatu ilikuwa imewekwa pakiti za unga mweupe unaosadikiwa kuwa wamethaqualone au mandrax, dawa ambayo hutumiwa kama mbadala wa cocaine, imeandika tovuti hiyo.

Kamanda wa Kikosi cha Kupambana na Madawa ya Kulevya nchini, Godfrey Nzowa alisema kwa kuwa mwanamke huyo amekamatwa nchini India,Tanzania haiwezi kuingilia kwa undani ingawa wanasubiri iwapoIndia watawapigia simu.

"Kila nchi ina sheria yake na ina uwezo wa kumchukulia hatua Fatuma kwa kuwa yupo ndani yanchi hiyo,"alisema.

Nzowa alisema nchi nyingi duniani zipo kwenye vita dhidi ya dawa za kulevya hivyo hashangai kwa Mtanzania huyo kukamatwa nchini India.

Nzowa alisema dawa hizo ni kemikali au vibashirifu vinavyotumika kutengeneza dawa za kulevya na huzalishwa zaidi India.

Alisema ephedrine zinatumika kutengenezea dawa za kikohozi lakini kinachojitokeza watu wanabadilisha matumizi yake na kutengeneza dawa za kulevya.

Nzowa alisema aina hiyo ya vibashirifu inalimwa kihalali nchini India kwa vibali maalumu kwa ajili ya kutengenezea dawa ya kikohozi,

Chanzo:Mwananchi

MKENYA, MRUNDI JELA MWAKA MMOJA KWA WIZI WA GARI LA MAFUTA

RAIA wa Kenya na mwingine wa Burundi waliokuwa wakikabiliwa na kesi ya wizi wa gari na mafuta ya petroli wamehukumiwa kwenda jela mwaka mmoja kila mmoja, huku Watanzania watatu wakiachiwa huru kwa kukosekana ushahidi.

Kesi hiyo ilikuwa ikiwakabili raia wa Kenya, Said Abeid na wa Burundi, Garuka Haruna na Watanzania walioachiwa huru ni mfanyabiashara Bundala Kapela, Juma Kasago na Rashidi Juma.

Walihusishwa na wizi wa petroli ya thamani ya Sh milioni 100 na gari lenye thamani ya Sh milioni 200. Walitiwa hatiani na Mahakama ya Hakimu Mkazi wilaya ya Igunga mjini Tabora nchini.

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu mkazi Wilaya, Ajali Milanzi alisema mahakama imewatia hatiani washitakiwa namba tatu, Abeid na Haruna kutokana na kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo.

Mahakama hiyo imewahukumu kwenda jela mwaka moja kila mmoja huku ikizingatia kuwa watuhumiwa hao walikaa mahabusu zaidi ya miezi minane.

Hakimu Milanzi alisema washitakiwa Kapela, Juma na Kasago wameachiwa huru baada ya mahakama kutowakuta na hatia dhidi ya tuhuma hizo za wizi wa mafuta na gari.

Awali Mwendesha Mashitaka wa Jeshi la Polisi Wilaya ya Igunga, Elimajidi Kweyamba, aliiambia mahakama hiyo kuwa Septemba mwaka 2014 saa 8:00 mchana katika kijiji cha Ziba, watuhumiwa hao waliiba gari lenye namba za usajili RAC 3542 likiwa na tela yake namba RL 0635 lenye thamani ya Sh milioni 200.

Gari hilo lilikuwa na mafuta lita 43,000 yenye thamani ya Sh milioni100, vyote vikiwa na jumla ya thamani ya Sh milioni 300 mali ya kampuni ya Merries ya Kigali, Rwanda.

MTOTO WA MKULIMA ACHUKUA FOMU, ASEMA ATAFANYA MAMBO KIMYAKIMYA

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amekuwa kada wa 31, kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa na CCM kugombea urais, huku akijigamba kwa mafanikio ya serikali iliyopo madarakani.

Pinda maarufu kama "mtoto wa mkulima" alisema hawezi kusema atafanya nini bali atakachokiangalia ni ilani ya CCM, na hataanzisha jambo jipya bali kuendeleza pale serikali ya awamu ya nne ilipoishia.

Akitangaza nia baada ya kuchukua fomu katika ofisi za Makao Mkuu ya CCM, mjini Dodoma, alisema anafanya mambo kimya kimya na hatangazi kama wengine wanavyofanya na kwamba kwa upande wa miundombinu ambayo inafanya vizuri ni kwa sababu yeye ni kiranja wa mawaziri husika. Kaulimbiu yake ni "Wanyonge sasa tuwainue" na kusisitiza amesema hivyo kwa kuwa mpango wa pili wa maendeleo utayagusa makundi hayo.

"Uchungu wa mwana aujuaye mzazi, nimesema hivi makusudi, mimi ndiyo nipo serikalini hivi sasa, kamani uchungu wa mwana mimi naujua zaidi," alisema.

ILANI YA CCM
Pinda ambaye alijitapa kuwa ni mtoto wa serikali za mitaa, alisema CCM ina utaratibu mzuri kwani hakuna anayeweza kusimama na kusema lolote bali wanaongozwa naIlani na kwamba haijatoka hivyo hawezi kusema atakayofanya.

"Ndani ya Ilani kuna maelekezo yote, sera, mikakati na maelekezo ikiwamo kuahidi Watanzania nini atawafanyia kwa miaka mitano, kwa sababu haijatoka sina la kusema, nachoweza kuahidi ikikamilika na kupitishwa na mkutano mkuu na Mungu kunitambua, sitashindwa kutekeleza ilani hata kidogo," alibainisha.

"Nalisema kwa kujiamini kwani nimekuwapo serikanili kwa muda mrefu, nimefanya kazi na Mwalimu Julius Nyerere, Ali Hassan Mwinyi kwa miaka kumi, Benjamini Mkapa kama Naibu Waziri na sasa nipo na Jakaya Kikwete kwa miaka nane, hawa pia ni viongozi wa chama hiki na wanasimamia ilani itekelezwe, nimejifunza mengi, pia mimi ndiyo msimamizi wa ilani."Alisema mambo makubwa ni usimamizi ni uwajibikaji, kupambana na rushwa, kilimo.


DIRA YA MAENDELEO
Alisema katika utelekezaji wa Ilani ya chama chake ni lazima kutelekeza Dira ya Maendeleo ya 2000 -2025, mwaka 2005.

Pinda ambaye ametajwa kwenye kinyang'anyiro hicho kwa muda mrefu, alisema Rais Kikwete alionekana kuongeza nguvu kwenye eneo hilo, na Kikwete alianzisha Mpango wa Maendeleo ili kuitekeleza Dira ipasavyo ambayo inataka ikifika mwisho Tanzania iwe nchi ya uchumi wa kati.

Alisema ndani ya Dira siyo rahisi kuona mambo yote kwa kuwa ni sera ya jumla na ndipo ulipozaliwa mpango wa maendeleo uliogawanyika katika miaka mitano mitano, na wa kwanza utakamilika mwaka huu.


NINI KIMEFANYIKA
Alisema ndani ya miaka mitano ilikuwa ya kufufua na kujenga mambo muhimu ambayo ni miundombinu ya barabara, reli na bandari.

"Mkapa alianza Kikwete akaendeleza ndani kuna program ya ujenzi wa barabara inayotakiwa kumalizika 2018, kuwe na mtandao wa barabranchi nzima kuunganisha makao makuu ya kila mkoa kwa barabara za lami."

"Anachokifanya Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, ni utekelezaji wampango wa miaka mitano na jingineni mkakati wa kupunguza umaskini ni program ndani ya mpango na hivi karibuni wataanza kuandaa mpango wa pili wa maendeleo wa miaka mitano utalipeleka taifa hadi 2021 ili ikifika 2025/26 ili kutekeleza Dira."Alisema kinachotarajiwa kufanyika kwa miaka mitano ijayo ni kujenga uwezo wa kiuchumi kwa kujenga viwanda na msisitizo ni viwanda vyausindikaji wa mazao yanayotokana na wakulima, wafugaji na wavuvi.


MAADUI
Alisema maadui wakubwa wakati wa Mwalimu Nyerere ni umaskini, ujinga na maradhi, lakini kwa marais watatu waliopita walibainisha maadui wakubwa wengine uharibifu wa mazingira na utawala bora.

Alisema uchumi imara utawezesha kumaliza maadui ujinga, maradhi naumaskini, huku uharibifu wa mazingira utafanikiwa kwa kuelimisha umma kwa kujenga fikra mpya namna ya kuhifadhi misitu navyanzo vya maji.


UTAWALA BORA
Alisema unawataka Watanzania wote kutambua tuna wajibu kuhakikisha nchi iendeshe mambo yake kwa uwazi, viongozi waadilifu watakaolivusha taifa, kiongozi ambaye kila akikaa anajua watu wake ni maskini anatakiwa kuwainua.
"Wanatueleza mmnefanya vizuri lakini umaskini umepungua kwa kiasi kidogo sana asilimia 28, tunataka mshuke zaidi…wanasema tatizo lenu ukuaji wa uchumi umetegemea sekta ya ujenzi, maliasili, uchukuzi, mchangowake ni mkubwa lakini haugusi jamii kubwa moja kwa moja.

"Alisema wanachotakiwa kufanya kwa sasa ni kupeleka jitihada hizo kwa wakulima, wavuvi na wafugaji kwa kutumia malighafi kutoka kwa makundi hayo na hivyo kupunguza umaskini kwa kasi kubwa.


KILIMO
Alisema kinachokimbiza watu kwenye kilimo ni jembe la mkono na kinachotakiwa ni vifaa vya kisasa,na hivyo ndani ya miaka mitano ijayo hali za maisha ya watu wa chini zitainuka.

"Kama Mwenyezi Mungu itampendeza nikawa mmoja wa waliochaguliwa, ni eneo piga geuza, kufa na kupona nitalisimamia kwa nguvu zangu zote," alisisitiza na kuongeza: "Wapo ambao hawataki kusikia hata na kusema ni mambo ya Kikwete, kinachotakiwa ni kuyabeba na kuyasukuma kwa kuwa msingi upo, tukienda hivi ndani ya miaka kumi Tanzania itabadilika."Aidha, aliwataka viongozi na Watanzania kutobeza juhudi za Kikwete.

RUSHWA
Pinda ambaye pia ni Mbunge wa Katavi, alisema lazima serikali izingatie utawala bora kwa kupambana na rushwa na uovu wowote wenye kulirudisha nyuma taifa kimaendeleo.


SERIKALI ZA MITAA
Alisema amekuwapo serikali za mitaa tangu aingie serikalini na kwamba hati chafu zimepungua kutokana na usimamizi wa karibu alioufanya.

Alisema yeye (Pinda) ndiye mtu sahihi kwani mtu mpya atahitaji muda wa kujifunza, kuelewa na kuuliza na wakati mwingine ataboronga.


MASHANGINGI
Pinda alisema serikali imepunguza magari ya kifahari aina ya VX8, ambayo gari moja ni zaidi ya Sh milioni 300, ambayo inawezesha upatikanaji wa magari mawili au matatu.

Waziri Mkuu aliambatana na wabunge na viongozi wengine ambao ni Dk. Cyril Chami, Martha Mlata, Dk. Orudencia Kikwembe, Dk. Peter Kafumu, Meya wa Jiji la dar es Salaam, Didas Masaburi, aliyewahi kuwa mbunge, Dk. Christan Mzindakaya, aliyekuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Moshi, Berbadetta Kinabo.

UJERUMANI: WAHAMIAJI NI MUHIMU

Maafisa nchini Ujerumani wanasema kuwa idadi inayozidi kuongezeka ya wakimbizi wanaowasili kutoka nchini kama syria watasaidia kujaza pengo la ukosefu wa wataalamu.

Mwenyekiti shirika la ajira nchini Ujerumani aliliambia gazeti mojakuwa watu wanaokimbia syria, wengine wameelimika na hivyo wanakaribishwa nchini Ujerumani.

Wakimbizi 350,000 watarajiwa kutafuta ajira nchini ujerumani mwaka huu.

Ujerumani hupokea maombi mengi ya hifadhi kuliko nchi yoyote katika muungano wa ulaya na idadi hiyo inazidi kuongezeka.

MAJAMBAZI YAUA ASKARI MPELELEZI MBEYA

Majambazi yamemuua polisi wa upelelezi, William Mtika (29) wa jijini hapa wakati wa mapambano kwenye tukio la kutaka kupora fedha za Kampuni ya Export And Trading eneo la Iwambi.

Tukio hilo lilitokea juzi saa 9:00 alasiri na katika mapigano hayo, jambazi mmoja alipigwa risasi mguuni na baadaye kufariki dunia kutokana na kuvuja damu nyingi.

Akizungumza wakati wa kuaga mwiliwa marehemu huyo, Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Ahmed Msangi alisema Mtika akiwa na askari wenzake walipata taarifa za watu waliotiliwa shaka nyendo zao eneo hilo ndipo wakaelekea kwenye tukio.

"Askari wakiwa eneo la tukio walifanikiwa kuwakamata majambazi waliokuwa kwenye pikipiki baada ya kugonga gari la Polisi kabla ya nyingine kutokea na kuwapiga risasi ambazo moja ilimpata askari wetu Mtika," alisema.

Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Nyerembe Mnasa aliwataka polisi kutorudi nyuma katika mapambano, huku akiwasisitiza wananchi kutoa taarifa za watu wanaowatilia shaka katika maeneo yao.

Mwili wa marehemu Mtika uliagwa jana mchana nyumbani kwake eneola Ghana Mbeya na kusafirishwa kwenda mkoani Mara kwa ajili ya mazishi.

Alisema polisi pia walifanikiwa kukamata bastola moja iliyotengenezwa kienyeji inayotumia risasi za Shotgun na pikipiki mbili.

Akifafanua chanzo cha tukio alisema, awali majambazi walimvamia mfanyakazi wa kampuni aitwaye Madhu Basavaranjappa lakini alipiga risasi juu ambazo ziliwafanya nao wajibu na hatimaye kuamua kukimbia na ndipo walipokutana na polisi.

Kamanda Msangi alisema wanaendelea na msako mkali wa kuwatia nguvuni majambazi hao huku akisisitiza kwamba kifo cha polisi wake katu hakitawavunja moyo polisi bali kitaongeza morali kuhakikisha wanapambana na aina yoyote ya uhalifu.

Chanzo: Mwananchi

BAJETI AFRIKA MASHARIKI ZASOMWA

Serikali za Afrika mashariki zimetumia kodi kuvitahadharisha viwanda vyake kwa upande mmoja na kuwapa motisha wananuzi wa bidhaa kutoka nje wanaosaidia sekta muhimu kama vile miundo mbinu, kawi mbali na utekelezwaji wa itifaki ya soko la pamoja.

Katika mapendekezo ya bajeti yaliosomwa siku ya alhamisi Kenya, Uganda Rwanda na Tanzania zimepunguza kodi za bidhaa zinaozoagizwa kutoka nje kwa sekta muhimu kama vile kawi,mawasiliano na miundo mbinu.

Kulingana na gazeti la the east African nchini Kenya, shinikizo la kuimarisha miundo mbinu, kupunguza gharama ya kufanya biashara na kuongeza mtiririko wa mapato kutoka kwa mafuta na gesi iliogunduliwa katika eneo la Afrika mashariki umeyafanya mataifa manne ya eneo hili kushusha masharti ya sera za kodi ili kurahisisha biashara na majirani zao pamoja na mataifa ya kigeni.

Rwanda imepunguza kodi katika magari yanayoagizwa kutoka nje hususan matinga tinga, malori pamoja na mabasi ya uchukuzi.

Tanzania kwa upande wake imechukua mkondo kama huo na kupunguza kodi ya kuagiza bidhaa kutoka nje kutoka asilimia 25 hadi 10 miongoni mwa mabasi yanayobeba abiria 25 kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Uwiano wa kikanda unalenga kurahisisha biashara na kuzuia hasara inayokumba kampuni zinazofanya biashara katika eneo hili.

Hatahivyo, wafanyibiashara katika mataifa kama vile Rwanda na Uganda wanalazimika kulipia hasara inayotokana na masharti ya kibiashara yaliowekwa na wasanifu.

Ili kuondoa matatizo hayo Kenya imetangaza kuwa inapunguza masharti kadhaa ya kibiashara kupitia kuondoa forodha ya usalama katika uagizaji wa sukari ya viwanda na unga na ngano.

Uganda nayo imechukua mkondo huo kwa kuondoa forodha yake ya usalama kwa bidhaa na kuanzisha mtindo wa kulipa unaojulikana ambao unalenga kuleta uwiano.

LIPUMBA KUCHUKUA FOMU YA URAIS

Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), Prof. Ibrahim Lipumba (pichani), Jumapili anatarajiwa kuchukua fomu ya kugombea urais.

Mkurugenzi wa Mipango na Uchaguzi wa CUF, Shaweji Mketo, alisema jana kuwa mchakato wa kutangaza nia ya kugombea urais ulianza Mei 10 hadi Juni 10, mwaka huu na kuwa hadi kufikia jana ambayo ilikuwa siku ya mwisho walikuwa wamepokea jina Lipumba pekee.

"Mchakato wa utangazaji nia ya kugombea ndani ya chama ulifunguliwa Mei 10 na hadi kufikia jana, tumepokea jina la Prof. Lipumba tu katika ngazi ya urais," alisema.

Aidha, alisema walipanga wagombea waliotangaza nia ya kugombea urais kuchukua fomu kuanzia Juni 11, mwaka huu, lakini kwa kuwa mgombea mmoja ndiye amejitokeza wakapanga Juni 14, 2015 iwe siku ya mwisho kuchukua fomu kwa ngazi hiyo.

Alisitiza kuwa wananchama na wananchi wanatakiwa kujitokeza kwa wingi kwenda kumsikiliza Prof. Lipumba ambaye ataeleza kwa nini amechukua fomu kugombea urais.

Aliongeza kuwa Baraza la Kuu la Uongozi la chama hicho linatarajiwa kukutana Julai 11 na 12, mwaka huukwa ajili ya uteuzi wa mwisho wa wagombea katika ngazi ya ubunge na urais na kuwa hadi Julai 20, mwaka huu vyama vyote vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vimekubaliana viwe vimemaliza kuteua wagombea ambao watapitishwa katika vikao vya Ukawa.

Mketo alisema katika majimbo 189 ya Tanzania Bara, tayari wameshapata wagombea waliotangaza nia ya kugombea kwenye majimbo 133 wakati 56 bado hayajatangaziwa nia.

CHANZO: NIPASHE

MAKAMBA: NISIPOTEULIWA SITAKUWA NA KINYONGO

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba, ambaye anawania uteuzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kugombea urais, ameahidi kuwa asipoteuliwa hatakuwa na kinyongo na atarejea kukijenga chama.

Aidha, ameahidi kuwa atalirudisha Jimbo la Iringa Mjini mikononi mwaCCM.

Jimbo hilo kwa sasa linaongozwa na Mchungaji Peter Msigwa, wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Kadhalika, Makamba amemwaga ahadi lukuki kwa wakazi wa mji wa Iringa ikiwamo kuwasaidia vijana wabodaboda, kupanua uwanja wa ndege mkoani humo, kujenga barabara ya lami kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Ruaha pamoja na kufufua viwanda.

Ahadi nyingine ni pamoja na kuhakikisha vijana wanaojiunga na vyuo vikuu, wanapata mikopo bila usumbufu wowote kwa kuwa kupata elimu ni haki yao.

Aliyasema hayo jana alipozungumzana makada wa CCM, kutoka wilaya zote za mkoa wa Iringa, alipokuwa akitafuta wanachama wa kumdhamini.

Makamba alipata zaidi ya wadhamini 600 ambao ni zaidi ya idadi inayotakiwa na chama ambayoni wanachama 30 kwa kila mkoa.

Aliongeza kuwa mchakato wa kumpata mgombea, hauna uhasamana kwamba hata kama kushinda ama kushindwa atakuwa mtu wa kwanza kuanza kukijenga chama upya ili kurudisha mshikamano.

"Mimi nitakuwa mtu wa kwanza kuanza kukijenga chama baada ya uchaguzi mkuu, wanachama wote wanatakiwa kukaa kama familia moja ili kujenga mshikamo pamoja na kujadili makovu ya uchaguzi," alisema.

Makamba alisema ana imani kwamba CCM kitapitisha mgombea kwa kujiamini bila kuogopa kusambaratika na wala wanachama wasisikilize watu wanaojipitisha mitaani na kusema kwamba chama kitasambaratika baada ya uchaguzi.

Kabla ya kukutana na wanachama wa CCM katika ofisi za wilaya, Makamba alisema Iringa ni kama nyumbani kwao kwa kuwa aliwahi kuishi hapo wakati baba yake akifanya kazi mkoani humo.

Wakati wa mapokezi yake, vijana waendesha bodaboada waliongoza msafara wake, huku wakiimba nyimbo hadi katika ofisi za wilaya ambako alikabidhiwa majina ya makada waliomdhamini.

Kutokana na wingi wa wananchi wakiwamo makada wa CCM, uongoziwa wilaya wa CCM, ulilazimika kuwaomba watu watoke nje ya ukumbi ili wakutane na Makamba eneo la wazi azungumze nao.

JACK WARNER ALIA MAREKANI INALIPA KISASI

Aliyekuwa makamu wa rais wa shirikisho la Soka Duniani FIFA, Jack Warner, ameituhumu Marekani kwamba inafuatilia mashtaka ya rushwa dhidi ya maafisa waandamizi wa shirika hilo kwa sababu imeshindwa kuwa mwenyeji wa kombe la dunia la mwaka 2022.

Akiandika katika gazeti ambalo analolimiliki huko Trinidad na Tobago, bwana Warner amesematuhuma hizo dhidi yake na wengine kumi na tatu zinaonyesha kwamba Marekani inaegemea upande mmoja.

Warner amekana tuhuma hizo. Shirikisho hilo la Soka Duniani limegubikwa na tuhuma za rushwa kwa kipindi cha wiki mbili mfululizo. Akiandika katika gazeti lake linaloitwa Sunshine, Warner anaelezea mashtaka ya Marekani dhidi yake kuwa ni uonevu na yaliyoegemea upande mmoja.

Warner amesema Marekani ambayo inajifanya kuwa ni polisi wa dunia, imehamasika kuchukua hatua hiyo baada ya kushindwa kuwa mwenyeji wa mashindano ya kombe la dunia ya mwaka 2022.

Warner, mwenye umri wa miaka 72 amekana tuhuma za kupokea rushwa ya dola milioni kumi za kimarekani kutoka Afrika Kusini baada ya kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa michuano ya kombe la dunia ya mwaka 2010.

Katika makala yake, Warner ameendelea kujitetea kwa kusema kuwa, kuishutumu AfrikaKusini kunachafua hadhi ya hayati Nelson Mandela ambaye ameisaidia Afrika Kusini kupata nafasi hiyo.

Gazeti hilo limeonyesha picha za Jack Warner akikutana na Prince William, David Beckham, Barack Obama na Vladimir Putin ambao amesema wote walikuwa na ushawishi pindi nchi zao zilipokuwa zikifanya kampeni ya kuwa mwenyeji wa Kombe la Dunia.

Jack Warner amemalizia kwa kuuliza iwapo walikuwa wanatumia takrima kama rushwa?

Jack Warner ni mmoja wa maofisa wa ngazi za juu wa bodi ya shirikisho la soka duniani FIFA, ambao wanatuhumiwa kwa kashfa ya rushwa na mpaka sasa Warner amekana tuhuma zote zinazomkabili.

WAGOMBEA URAIS WAINGIA MITINI KWENYE MDAHALO

WAGOMBEA urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), juzi walikimbia mdahalo wa kupambana kwa hoja ulioandaliwa na wenyeviti wa sekta binafsi na kujulikana kama 'CEO round table of Tanzania'.Mdahalo huo ulikuwa na lengo la kujadili mambo makuu mawili, ikiwa ni sekta ya uchumi na utawala bora na kwa jinsi gani wagombea hao wakipata ridhaa ya kuliongoza taifa, wangetekeleza vipaumbele hivyo katika kuliletea taifa maendeleo.

Akizungumza mara baada ya kuahirisha mdahalo huo, Mwenyekiti wa Mdahalo, Ally Mfuruki alisema amesikitishwa sanana wagombea hao kwa kushindwa kuhudhuria kwenye mdahalo huo, kwani hadi muda unakaribia wa kuanza majadiliano, walitoa taarifa za kuhudhuria.

"Nashindwa hata kuelewa ni sababu zipi zimewafanya hawa wagombea wasifike kwani muda mfupi tu uliopita niliwasiliana nao na wakasema wanakuja, lakini baada yakuona muda unaenda na hakuna aliyefika, nikapata taarifa kuwa hawatafika na sijapewa ni sababu zipi zimewakwamisha," alisema Mfuruki.

Waliotarajiwa kuhudhuria mdahalo huo ni Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, Naibu Waziri wa Mawasiliano January Makamba, Balozi Amina Ally, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu na Waziri Mkuu mstaafu, Frederick Sumaye.

Alisema anashangaa kutojitokeza kwao na kuwa aliyejitokeza ni mgombea mmoja tu, mwanamke pekee katika kinyang'anyiro hicho cha kuwania kiti cha urais, ambaye ni Balozi Amina Ally.

Lakini, alithibitisha kupokea taarifa za kutohudhuria kwa Waziri Nyalandu na kusema kuwa alipata dharura ya kikazi na hivyo alitoa taarifa ya kutohudhuria mapema na Sumaye pia alipata dharura na kutoa taarifa ya kutokuwepo kwenye mdahalo.

Kwa upande wake, Balozi Amina Ally alisema anasikitishwa na wagombea wenzake kwa kutoitika wito wa kuhudhuria, kwani wananchi wanachokitaka ni kuwafahamu kwa undani wagombea kwa kupitia midahalo na kuweza kutambua ni yupi atakayewaletea maendeleo na kuwatatulia changamoto zinazowakabili.

AUAWA KWA KIPIGO JWA KUPINGA MAMA YAKE KUOLEWA NA KIJANA

MKAZI wa kitongoji cha Izia, manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa, Sylvester Mtoni (32) ameuawa kikatili na baba yake wa kambo wakishirikiana na bibi yake baada ya kushambulia kwa ngumi, mateke na rungu.

Mtafaruku huo ulitokea baada ya marehemu kuamua kumfukuza baba yake huyo wa kambo anayefahamika kwa jina moja la Bea mwenye umri wa miaka 32 akipinga uamuzi wa mama yake mzazi kuishi nae kinyumba katika nyumba aliyoijenga marehemu baba yake.

Inaelezwa kuwa wakati mkasa huo ukitokea mama mzazi wa marehemu alikuwa safarini akielekea jijini Dar es Salaam.

Inadaiwa kuwa mtoto huyo alimkatalia mwanamume huyo kumwoa mama yake mzazi kwa kuwa ni kijana mwenzake umri wao ukilingana ambao ni nusu ya umri wa mama yake mzazi.

Akithibitisha kutokea kwa mkasa huo Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoawa Rukwa, Leonce Rwegasira alidai kuwa ulitokea juzi usiku katika kitongoji cha Izia Manispaa ya Sumbawanga.

Alieleza kuwa chanzo chake ni kuwa marehemu alipinga uamuzi wa mama yake mzazi kuolewa na mwanaume ambaye ana umri sawa na yeye (Sylivester) na kuishi katika nyumba aliyoijenga marehemu baba yake.

"Usiku huo wa tukio mtuhumiwa ambaye anatafutwa na jeshi la polisi alimshambulia mwanawe huyo wa kambo akisaidiwa na mama mkwe wake wakimpiga kwa ngumi matekena kipande cha ubao hadi kijana huyo alipopoteza fahamu," alieleza Kaimu Kamanda Rwegasira.

Akifafanua aliongeza kuwa alikimbizwa Hospitali ya Mkoa ambapo alikufa akiwa anaendelea na matibabu hospitalini hapo.

MKULIMA WA DARASA LA SABA AUTAKA URAIS

KATIKA hali isiyo ya kawaida, mkulima kutoka Kijiji cha Mjimtala Wilaya ya Kasulu Mkoani Kigoma, Eldoforce Bilohe (43) jana alitinga makao makuu ya Chama Cha Mapindizi (CCM) kuchukua fomu ya kuomba ridhaa kuteuliwa kuwa mgombea urais, bila kuwa na ada huku akiwa amebeba maji ya chupa kwapani.

Bilohe ambaye alisema elimu yake ni ya darasa la Saba, aliwasili makaomakuu ya CCM muda wa saa 5:40 asubuhi na kuelekea Ofisi ya kupokea wagombea ndani ya ofisi baada ya kuwapita waandishi wa habari wakiwemo wapiga picha, waliokuwa wamejipanga kumsubiria, lakini aliwapita waandishi bila kumtambua kuwa ni mgombea,

Akiwa amevaa suruali ya kaki na fulani yenye rangi ya kijani na njano, alionekana kuduwaza watu wengi, ambao walikuwa wakiwasuburi wagombea, ambao walikuwa wakichukua fomu jana.

Akiwa kati ya watu waliokuwa kwenye orodha ya kuchukua fomu, Bilohe alikuwa amebeba chupa ya maji kwapani baada ya kufika na kupokelewa na maafisa, ambao walimtambua kuwa ni mgombea na ndipo wapiga picha waligutuka na kuanza kupiga picha.

Kisha aliingia ndani ya ofisi ya kuchukua fomu na alitoka baada ya muda mfupi na kuanza kuhojiwa na waandishi wa habari.

Alisema amefika Dodoma kwa ajili ya kuchukua fomu ya kuteuliwa kuwa mgombea urais, lakini kwa sababu ambazo hazijafahamika, aliambiwa akachukue fedha.

"Nilipigiwa simu wakati niko benki ya CRDB nikiwa kwenye foleni, nikisubiri kuchukua fedha, ndiyo nikakimbia kuja hapa," alisema.

Alisema amekuwa mwanachama haiwa CCM tangu mwaka 2003 na elimu yake ni ya msingi na ana uzoefu kutokana na kuwa katika chama kwa muda mrefu.

"Nimekuja kama nilivyo kwa sababu sijawahi kuwa na makundi unayoyaona wewe, mimi ni mwanachama wa kawaida kama wanachama wengine," alisema.

Mmoja wa maofisa wa chama, ambaye hakutaka kutaja jina lake, alisema Bilohe amerudisha si kwa sababu hana hela, bali kuna vigezo ambavyo havijafikiwa, ikiwemo barua ya utambulisho kutoka kwa Katibu wa CCM Wilaya aliyotoka.

"Hajakamilisha taratibu za kumwezesha kuhukua fomu," alisema.

Hata hivyo, taarifa zilizopatikana baadaye zilisema kuwa tayari mkulima huyo ameshalipia ada ya fomu ya Sh 1,000,000 na atachukua fomu yake leo saa 10 jioni.

BVR YABAINI 152 KUJIANDIKISHA ZAIDI YA MARA MOJA

Watu 152 wamebainika kujiandikisha zaidi ya mara moja kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura kwa mfumo wa Biometric Voters registration (BVR) katika mikoa mitano iliyokamilisha uandikishaji huku Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) ikiahirisha uandikishaji wapigakura kwa wiki moja kuanzia jana katika mikoa minne.

Mikoa ambayo uandikishaji umeahirishwa kuanzia jana hadi Juni16, mwaka huu ni Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Mara.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana na waandishi wa habari kuhusiana na uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapigakura unavyoendelea, Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Nec, Dk. Sisti Cariah, alisema watu hao waliobainika kujiandikisha zaidi ya mara moja watachukuliwa hatua.

"Kwa mujibu wa sheria, hilo ni kosa la jinai na kwa hiyo tutawachukulia hatua za kisheria mara moja na kwahali hiyo ninawaasa wananchi kuachana na udanganyifu huo, kwani mfumo wetu tulionao utawatambua mara moja," alisema.


KUAHIRISHA MIKOA MINNE

Kuhusiana na kusogezwa mbele kwawiki moja uandikishaji wa wapiga kura katika mikoa hiyo minne, Dk. Cariah alisema imetokana na mabadiliko ambayo yanaendelea kufanywa ya mipaka ya kiutawala yakata, vijiji, vitongoji na mitaa.

Alisema mabadiliko hayo yanatakiwa kufanyiwa kazi katika mfumo mzima wa Daftari la Wapigakura kwa mikoa hiyo minne na hasa ikitiliwa maanani kuwa katika mabadiliko hayo, kata 130 mpya zimeongezeka.

Alisema katika maeneo ambayo shughuli ya uandikishaji imeshafanyika, Nec itafanyia mabadiliko katika mfumo wake baadaye.


NEC YAFIKIA LENGO

Aidha, Dk. Cariah alizungumzia namna Nec ilivyofikia lengo lililotarajiwa la kuandikisha wapigakura katika mikoa mitano ilikomaliza kazi hiyo ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Iringa na Njombe.

Alisema katika mkoa wa Lindi, idadiya watu walio na umri wa miaka 18 hadi kufikia siku ya kupiga kura iliyotarajiwa kuandikishwa kwa mujibu wa Ofisi ya Takwimu ya Taifa(NBS) ilikuwa ni 518,230, lakini Nec ilifanikiwa kuandikisha wapiga kura 529,224 sawa na asilimia 102.

Kwa upande wa Mkoa wa Mtwara, Nec ilitarajia kuandikisha wapiga kura 732,465, lakini iliandikisha wapiga kura 727,565 sawa na asilimia 99.

Alisema kwa upande wa Mkoa wa Ruvuma, Nec ilitarajia kuandikisha wapiga kura 783,296, lakini ikaandikisha wapiga kura 826,779 sawa na asilimia 106, na kwa Iringa, Tume ilitarajiwa kuandikisha wapiga kura 524,390 lakini ikaandikisha wapiga kura 526,006 sawa na asilimia 101.

Hata hivyo, alisema kwa Mkoa wa Njombe ambao ulikuwa wa kwanza kuboresha daftari hilo, bado mawasiliano yafanyika kupata takwimu sahihi.

"Hivyo utaona kuwa utendaji wetu karibu unavuka malengo pamoja na wasiwasi ulioonyeshwa kupitia kwenye vyombo vya habari," alisema.

Vile vile, Dk. Cariah alisema Nec imepata mashine zote 8,000 za BVRambazo serikali ilikuwa imeahidi hadi sasa na kwa hiyo shughuli hiyo itakamilika kama ilivyopangwa.

"Niwahakikishie wananchi kuwa shughuli ya uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura litakamilika kabisa kufikia mwishoni mwa mweziwa saba," alisisitiza.


CHANZO: NIPASHE

DAESH WATANGAZA VITA DHIDI YA TALIBAN

Kundi la kigaidi la Daesh limetangaza vita dhidi ya kundila Taliban la nchini Afghanistan.

Shirika la habari la IRNA limemnukuu mkuu wa kundi la Daesh nchini humo, Abdurrahim Musallam Dust akisema kuwa, kundi la Taliban ni mwakilishi wa Shirika la Kijasusi la Pakistan ISI na ametangaza vita dhidi ya kundi hilo.

Kabla ya hapo, kundi la Daesh ambalo linaendesha vita katika nchi za Iraq na Syria liliwataka wanamgambo wa Taliban wajiunge na kundi hilo ili kupambana na kuangusha serikali za nchi hizo.

GAMBIA YAMTIMUA MWAKILISHI WA EU

Serikali ya Gambia imemtimua mwakilishi wa muungano wa Ulaya Agnès Guillaud kutoka nchini humo.

Amepewa saa 72 kuondoka nchini humo na hakuna sababu iliyotolewa ya kufukuzwa kwake.

Muungano wa Ulaya umekuwa ukiilaumu Gambia kwa ukiukaji wa haki za binadamu na mwaka uliopita ulizuia msaada wa karibu dola milioni 15 kwa nchi hiyo.

Shutuma nyingi zimeelekezwa kwa sheria zinazopinga mapenzi ya jinsia moja nchini humo.

MISRI: HAMAS SI KIKUNDI CHA UGAIDI

Mahakama nchini Misri imefuta hukumu ya awali ambayo ilikitajachama cha Hamas cha Palestina kama kikundi cha kigaidi.

Imefuta hukumu hiyo kwa sababu mahakama iliyotoa hukumu hiyo haikuwa na uhalali wa kufanya hivyo.

Misri inaonekana kama ni msuluhishi mwenye nguvu kwenye mzozo kati ya Israel na Hamas, ambayo inatawala eneo la ukanda wa Gaza.

Lakini tangu kuondolewa madarakani kwa rais Mohamed Morsi ,uhusiano baina ya Misri na Hamas umedondoka.

Hamas ilikuwa ni chama dada cha Muslim Brotherhood ambacho nichama cha rais Morsi.

Na sasa Muslim Brotherhood imepigwa marufuku nchini Misri.

MAMA AMCHOMA MWANAE KWA MADAI YA KUIBA UGALI

Stamili Mponzi mkazi wa kijiji cha Ikule wilayani Kilombero, mkoani Morogoro anashikiliwa na polisi kwatuhuma za kumchoma mwanae na kumjeruhi mikono kwa madai ya kuiba ugali.

Mama huyo alimuunguza mwanaye Joseph Chawala, akimtuhumu Kuiba Ugali, kwa mujibu wa watendaji mbalimbali wa kata ya Mng'eta.

Wakizungumzia tukio hilo Jerome Chulu na Jeneth Hetela, walisema unyanyasaji huo ulishuhudiwa na majirani wa mwanamke huyo baadaya kusikia kelele za watoto ambao walimchukua mtoto huyo kumpeleka ofisi ya mtendaji wa kata,polisi na baadaye hospitali.

Walibainisha baadaye kuwa polisi walikwenda kumkamata mwanamke huyo na mumewe Halidi Kiwenji ambaye inadaiwa alikuwa karibu wakati wa tukio hilo ingawa baadaye baba huyo aliachiwa ili akawaangalie watoto wengine nyumbani.

Polisi walithibitisha tukio hilo ambalo uchuguzi wake unaendelea ili kumfikisha mahakamani mtuhumiwa huyo.

Wananchi mbalimbali waliohojiwa wametaka hatua kuchukuliwà kwa watu wanaoendekeza vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.

WAZEE WOTE SASA KULIPWA PENSHENI ZANZIBAR

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) kuanzia mwaka huu wa fedha itawalipa pensheni wazee wote bila kujali kama waliajiriwa ama hapana.

Watakaonufaika na pensheni hiyo niwazee waliofikisha miaka 70 na kuendelea lengo la kufanya hivyo ni kuwawezesha kujikimu kimaisha.

Waziri wa Uwezeshaji Ustawi wa Jamii vijana Wanawake na Watoto Zainab Omar Mohamed akizungumza wakati akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo alisema mchakato wa kufahamu idadi ya wazee wote Unguja na Pemba wanaostahiki kulipwa pensheni hiyo umekamilika.

Alisema SMZ imechukuwa uamuzi huo ukiwa na lengo la kupambana na hali ngumu ya maisha inayowakabili wazee ambao baadhi yao hawakuajiriwa serikalini au na taasisi zake.

"Mheshimiwa Spika napenda kuwajulisha wajumbe wa Baraza la Wawakilishi (BWW)kwamba kwa mwaka wa fedha tutaanza kulipa pensheni kwa wote."alisema.

Aidha Waziri huyo aliwaambia wajumbe wa BWW kwamba juhudi za kupambana na matukio ya udhalilishaji wa kijinsia kwa wanawake na watoto zinaendelea ikiwamo kazi ya uzinduzi wa kampeni hizo iliyofanywa na Rais waZanzibar Dk.Ali Mohamed Shein.

Alisema kampeni hiyo ni muhimu kwa ajili ya kuhakikisha kwamba udhalilishaji unatokomezwa kwa kuzishirikisha taasisi mbali mbali pamoja na vyombo vya kusimamia haki na sheria.

Alieleza kuwa imebainika kwamba mapambano dhidi ya vitendo vya udhalilishaji wa kijinsia yanahitaji ushirikiano baina ya wizara ikiwamoya Katiba na Sheria, Elimu pamoja na Wanawake na Watoto.

Aidha alizitaka mahakama za Ungujana Pemba kuchukuwa juhudi ya kuharakisha hukumu kwa kesi za ubakaji kwani wananchi wameanza kuvunjika moyo kutokana na kesi hizo kuchukuwa muda mrefu hadi kutolewa kwa hukumu zake kwa kuwepo visingizio mbali mbali ikiwemo kukosekana kwa ushahidi.

"Tabia ya nenda rudi kesho imeanza kuwakatisha tamaa wananchi ambao wengine wanatoka vijijini kuja mjini kwa ajili ya kusikiliza kesiyake ambapo bila ya kupewa taarifaza uhakika kesi inaahirishwa"alisema.

Alisema baadhi ya kesi zinalazimika kufutwa na nyingine majalada yake kufungwa moja kwa moja kwa sababu zinakosa ushahidi muhimu ambao ndiyo utakaoweza kuwatia hatiani watuhumiwa wa makosa ukiwamo ubakaji.

DEREVA WA ROLI ASABABISHA AJARI, KUKATIZA RELINI WAKATU TRENI IKIPITA

Ubishi wa madereva wapitao barabara inayokatisha reli nusura igharimu maisha ya watu baada ya dereva wa maroli la mafuta lililokuwa likitokea mikoani kukaidi ishara ya mshika kibenedera wa shirika la reli na kusababisha ajali kubwa baina ya roli hilo na Treni.

Ajali hiyo imetokea majira ya saa tisa mchana na walioshuhdia ajali hiyo wameiambamia ITV kuwa kabla ya kutokea ajali hiyo dereva mwenye roli namba T.507 AVW lililokuwa na tera lake alisimamishwa kuahiria kuja kwa Treni lakini akakaidi hivyo kusombwa kisha kuburutwa na Treni umbali wa unaokadiriwa mita 60 pembeni mwa reli.

Alipoulizwa dereva wa Treni hiyo yenye namba 7321 aligoma katakata kuzungumza kwa madai kutokuwa na mamlaka ya kuongelea.

Mashuhuda walioshuhudia wamesema ukaidi wa dereva wa roli ndio uliochangia ajali hiyo lakini wakalilaumu shrika la reli kuacha kufunga barabara kwa vyuma inapotokea treni kuja na maafa kama hayo yamekuwa yakitokea mara kwa mara.

Katika hali ingine jeshi la polisi lililazimika kuifanya kazi ya ziada ya kuzuia watu wasikaribie tera la roli hilo wakihofia kutokea mlipuko kutokana na tera hilo kuhisiwa lilikuwa na mafuta na petroli.

Chanzo:ITV