ZAIDI YA WATU 1500 WAJITANGAZA KUWA MASHOGA IRINGA

Kukithiri kwa biashara haramu ya ngono pamoja na tabia ya ushoga mkoani Iringa kunadaiwa kusababishwa na baadhi ya vijana wa vyuo vikuu wanafika mkoani humo kwa ajili ya masomo ya elimuya juu, huku miongoni mwao wakitaka starehe zilizo nje ya uwezo wao.


Tamaa ya kumiliki vitu vya thamani – ni miongoni mwa mambo yanayotajwa kuwahadaa baadhi ya wasomi hao wa vyuo vikuu, jambo linalosababisha wengi wao kuangukia katika wimbi la biashara ya ngono na ushoga na kuufanya ongezeko la maambukzi ya vvu.


Kwa mkoa wa iringa inadaiwa kuwa zaidi ya mashoga 1500 wamejitangaza wenyewe kuendesha biashara haramu ya ngono, jambo ambalo kiafya linadaiwa kuwa ni hatari kwa maambukizi ya virus vya ukimwi.


Baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani iringa ndiyo wanaonyooshewa kidole kuhusika na biashara hiyo ya ngono na tabia ya ushoga- ambapo shirika la restless development linalojihusisha na masuala ya afya ya uzazi na makuzi kwa vijana- kupitia mradi wa dance for life- limewakutanisha viongozi hawa wa serikali ya wanafunziwa vyuo vikuu mkoani iringa- ili kujadili namna ya kujinasua katika wimbi hilo laushoga na biashara haramu ya ngono.


Serikali inaona tatizo hilo la ushoga na biashara ya ngono litamalizwa na jamii yenyewe, endapo tu wazazi na walezi watakemea mapema mienendo hatarishi ya vijana wao.


Ushoga ni tabia inayofanywa na baadhi ya wanaume, kwa kujihusisha kimapenzi na wanaume wenzao, suala ambalo kwa kiwango kikubwa linatajwa kuchochewa na mambo ya utandawazi, ambao unaibua mitindo mbalimbali na tabia mpya kila uchwao.