MWANDISHI WA MAREKANI ACHINJWA NA ISLAMIC STATE

Kikosi cha kiislam cha kijeshi chenye msimamo mkali kimeachilia video inayoonesha mauaji ya mwandishi habari mwenye asili ya Marekani. James Foley alipotea tangu alipokamatwa mateka na kushikiliwa nchini Syria miaka miwili iliyopita na sasa ameuawa.

Ikulu ya Marekani imesema inaifanyia uchunguzi wa kina video hiyo na ikithibitika kwamba mwandishi huyo wa habari ni wa taifa hilo ,serikaliya Marekani itataka ufafanuziwa kina ilikuaje na kwanini James Foley auawe.

Katika mtandao wa kijamii waFacebook familia ya mwandishi huyo iliandika kuwa 'tunajua kwamba wengi wenu mnasubiri uthibitisho ama majibu ya maswali yenu,tafadhalini muwe watulivu mpaka nasi sote tupate taarifa tunazo tamia,na tunaomba muendelee kumbumbuka Foleys na kumwombea kila siku.''

Katika video hiyo iliyobeba ujumbe unaosomeka kua ujumbe kwa Marekani, mwandishi huyo pia alionekana akiwa chini ya ulinzi wa mtu aliyekua amevalia kinyago usoni, askari huyo alikua aku akizungumza ndani ya lafidhi yenye athari za Uingereza, akisema kua kifo cha mwandishi huyo ni matokeo ya mashambulizi ya magurunedi yalowalenga wa Iraq.