Arfi Atupa Kadi Ya Chadema

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimezidi kuandamwa na
migogorobaada ya jana kuibuka mwingine mkubwa katika kikao chake cha
ndani mkoani Katavi kiasi cha kumfanya Makamu Mwenyekiti wachama hicho
Taifa, Said Arfi, kutupa kadi yake' Huu ni mgogoro wa pili mkubwa
kuripotiwakatika kipindi cha juma moja lililopita baadaya ule wa
wilayani Karatu ambako pamoja namambo mengine uliishia kwa Kamati
Kuusimamisha uongozi wote wa chama hicho wilaya. Taarifa zilizolifikia
gazeti hili jana zimeelezakuwa Arfi ambaye ni Mbunge wa Mpanda Mjini,
alitishia kujitoa Chadema jana, katika kikao cha Kamati ya Ushauri ya
chama hicho Mikoa ya Katavi na Rukwa kilichoketi Namanyere, Nkasi na
kufikia uamuzi wakumsimamisha Mwenyekiti wa Baraza laVijana Mkoa wa
Rukwa, Laurent Mangweshi.Katika kikao hicho, Arfi anadaiwa kuichukua
kadi yake ya Chadema na kumtupia Mwenyekiti wa Chadema Mkoa wa
Rukwa,John Mallack akitangaza kuachia nyadhifa zote alizonazo, kisha
kuondoka ukumbini kabla ya kufuatwa na wazee wa chama hicho na kumsihi
aichukue kadi yake hiyo. Alifikia hatua hiyo baada ya kutokea
sintofahamu kati ya wajumbe wa kikao hicho katika uamuzi huo
uliofikiwa kwa kupiga kura za ndiyo na hapana. Vyanzo vya habari
kutoka ndani ya kikaohicho vilifafanua kuwa Arfi alikerwa na kauli
iliyotolewa na Mangweshi kuwa katika Uchaguzi Mkuu uliopita, alipokea
rushwa kutoka kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Vyanzo hivyo vya habari
vimeeleza kuwa kutokana na hali hiyo, Arfi alipandwa nahasira na
kuamua kumrushia kadi Mallack kisha kutoka nje ya ukumbi. "Hatua hiyo
ilifanya wajumbe wa kikao hicho nao kutoka nje ya ukumbi na kuanza
kumbembeleza ili asichukue uamuzi huo nakisha wakamwekea kadi yake ya
uanachamakatika mfuko wake wa shati," alisema mmojawa makada hao. Arfi
mwenyewe hakupatikana jana kuzungumzia tukio hilo baada ya simu ya
mkononi kuita muda wote bila kupokewa nahata alipotumiwa ujumbe,
hakujibu. Mallack akizungumza na gazeti hili kwa simu alikiri Arfi
kurusha kadi mezani kisha kutoka nje ya ukumbi, lakini akasema suala
hilo lilishughulikiwa na wazee na kumalizwa."Ni kweli unajua huyu ni
Makamu Mwenyekitiwetu wa Taifa, sasa inapotokea vijana wadogo
wakamtuhumu kwa tuhuma za uongo na ambazo hazipo inatia hasira, ndiyo
maana huyo kijana tumemvua uongozi," alisemaMallack. Mangweshi
alisimamishwa uongozi baada yakutuhumiwa kwa mambo mbalimbali
yakiutendaji ndani ya chama hicho ikiwamo kumkashifu Arfi.Katika
mkutano wake na waandishi wa habari Mallack alisema kuwa Magweshi
amevuliwa uongozi baada ya chama hicho kujiridhisha kuwa alitenda
makosa hayo.Alisema kamati ya ushauri ilimwita ili kujibu tuhuma
mbalimbali zilizokuwa zikimkabili ikiwamo kutoa taarifa zisizo rasmi
bila kufuata taratibu za chama."Pia amepatikana na hatia ya kuandika
barua za kashfa na kuzipeleka makao makuu ya chama kumkashifu Arfi
pamoja na viongozi wengine wa chama akiwamo Katibu Mkuu Dk Willibrod
Slaa.Katibu Mwenezi wa Chadema Mikoa ya Rukwa na Katavi, John Matongo
alisema kabla yakupewa adhabu ya kusimamishwa amewahi kuonywa mara
kadhaa lakini ameshindwa kujirekebisha.



Chanzo: www.mwananchi.co.ctz

Ndege Ya Tanapa Yapata Ajali

Ndege inayomilikiwana shirika la hifadhi za taifa ya wanyama pori
TANAPA yenye usajiri wa namba 5H-FZS yapata ajari muda wa saa kumi na
dakika 50 wakati ikiruka kutoka uwanja wa ndege wa Mkoani Katavi
Wilaya ya Mpenda. katika Runway namba 027 mita 300 kutoka kwenye
Fence(Uzio) wa uwanja huo.
Ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria wanne, ni Rubani aliyejeruhiwa katika ajari hiyo na kuweza kupelekwa hospitali.
Picha: Nkwabi T. Kisanga

Askari Polisi Ajiuwa Baada Ya Kumjeruhi Mwanamke kwa Risasi

Kwa Habari zilizotufikia ni kuwa Askari Polisi wa Kituo cha polisi cha
mjini mpanda aliyeweza kufahamika kwa jina moja la Bwana Chacha
amefariki dunia baada ya kujipiga risasi kichwa hiyo imetokea baada ya
kumpiga risasi zinazokadiliwa kuwa mbili mwanamke ambaye walikuwa
wakigombea kiwanja walichouziwa, na tofari zilizo fyatuliwa kwenye
kiwanja hicho zadaiwa kuwa chanzo.

Wapigie Kura Washiriki Wa Maisha Plus Kutoka Katavi

Theresia katika pozi



Kumpigia Kura THERESIA ZAKARIA Andika MP01 kisha tuma kwenda No. 15584

Gabriel Lwinga

Katika pozi la picha

Lwinga
Kumpigia Kura GABRIEL LWINGA Andika MP18 kisha tuma kwenda No. 15584


Lucas

Lucas katika pozi

Kumpigia Kura LUCAS MARTIN Andika MP17 kisha tuma kwenda No. 15584

Wapigie kura washiriki hawa mara nyingi uwezavyo ili waweze kuibuka washindi ingawa mshindi ni mmoja lakini toa mchango wako kufanikisha kuleta taji mkoani Katavi, Katavi tunaweza


Picha: www.maishaplus.tv



Katibu Wa Bakwata Arusha Ajeruhiwa

Katibu wa BAKWATA Mkoa wa Arusha ABDULKARIM CHONJO amejeruhiwa vibaya
na amelazwa katika Hospitali ya Mount Meru baada ya nyumba yake
kulipuliwa na kitu kinachodaiwa kuwa ni bomu usiku wa kuamkia leo.

Source: ITV

JWTZ Wapita pita mitaani Kuangalia Usalama

Jeshi la wananchi wa Tanzania wakiongozwa na Jenerali Davis
Mwamunyange Wapita pita mitaa ya kariakoo kuangalia usalama yapatayo
magari makubwa matano yenye askari wapatao 20 kila gari walipita mitaa
hiyo. Huku Wafuasi wa shekh Ponda wataka kuelekea Ikulu kujisalimisha
huko, Askari wa kutuliza ghasia ndipo walipo anza kuwasambaratisha kwa
mabomu ya machozi.
Kwa sasa Askari wa JWTZ wapo maeneo ya Ikulu na wakati huu Rais Jakaya
Kikwete awasili kutoka Oman kwenye ziara yake.

JWTZ Wapita pita mitaani Kuangalia Usalama

Jeshi la wananchi wa Tanzania wakiongozwa na Jenerali Davis
Mwamunyange Wapita pita mitaa ya kariakoo kuangalia usalama yapatayo
magari makubwa matano yenye askari wapatao 20 kila gari walipita mitaa
hiyo. Huku Wafuasi wa shekh Ponda wataka kuelekea Ikulu kujisalimisha
huko, Askari wa kutuliza ghasia ndipo walipo anza kuwasambaratisha kwa
mabomu ya machozi.
Kwa sasa Askari wa JWTZ wapo maeneo ya Ikulu na wakati huu Rais Jakaya
Kikwete awasili kutoka Oman kwenye ziara yake.

Hali Si Shwari Jijini Dar Es Salaam

Hali imeendelea kuwa tete jijini dar es salaam, maeneo yote ya
kariakoo Posta maduka yamefungwa na imetangazwa kutokuwa na mkusanyiko
wa aina yoyote ule. Na inasemekana kuwa JWTZ wanaweza kuongeza nguvu
kwa polisi.

Hali Si Swari Jijini Dar Es Salaam

Hali imeendelea kuwa tete jijini dar es salaam, maeneo yote ya
kariakoo Posta maduka yamefungwa na imetangazwa kutokuwa na mkusanyiko
wa aina yoyote ule. Na inasemekana kuwa JWTZ wanaweza kuongeza nguvu
kwa polisi.

Uamsho Waamsha Tena

Vurugu kubwa zimevuka tena eneo la Darajan Visiwani zilizo sababishwa
na Kikundi chenye msimamo mkali cha Uamsho baada ya taarifa kuzuka
kuwa kiongozi wao ametekwa na watu wasio julikana, na Jijini Dar Es
Salaam polisi wamelazimika kuwatawanyisha watu waliokusanyika kituo
cha polisi jutaka shekh wao aachiwe baada ya kukamatwa jana usiku kwa
madai ya kuhusika na vurugu za hivi karibuni.

Kumbukumbu Ya Mwalimu

Tuangalie Baadhi ya hotuba za Mwalimu Nyerere alizozifanya wakati wa uhai wake.


Kumbukumbu Ya Mwalimu.

Ni miaka kumi na tatu tangu ututoke
Tuta kukumbuka kwa mambo yako yote, ulipinga ufisadi kukemea ukabila
na udini, kutoa elimu bure na mambo mengi


"Julius Kambarage Nyerere (13 April 1922 –14 October 1999) was
aTanzanian politician who served as the first Presidentof Tanzania and
previously Tanganyika, from the country's founding in 1961 until his
retirement in 1985.

Born in Tanganyika to Nyerere Burito (1860–1942), Chief of the Zanaki
Nyerere was known by the Swahili name Mwalimu, his profession prior to
politics. He was also referred to as Baba wa Taifa.


Pumzika kwa amani,

Kamanda Auwawa.

Kamanda wa mkoa wa Mwanza Ndugu Liberatus Barlow auwawa na majambazi
usiku wa kuamkia leo. Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi

Zurugu za Mbagala Kizuiani

Mkuu wa Dar Es Salaam,Said Meck Sadick,Kamanda wa Polisi kanda maalum
ya Dar Es Salaam Suleiman Kova na Sheikh wa Mkoa wa Dar Es Salaa,Alhaj
Musa Salum,wamewatak a waislam Jijini Dar Es Salaam kuacha Vurugu
zisizokuwa na tija kwakosa lililosababishw a na ubishani wa watoto
kuhusu Quran takatifu, jambo ambalo limesabaisha vurugu huko eneo la
Chamazi Mbagala ambapo magari yalivunjwa vioo na kuvunjwa kwa makanisa
Matatu.
Swali linakuja Makanisa yanausika na nini hapa?

Fujo Zazuka Mbagala

Fujo za zuka Mbagala na Polisi walazimika kutumia mabomu ya machozi
kutawanya wananchi Mbagala baada ya mtoto mmoja kumnyang'anya mwenzake
kitabu cha Dini ya kiislamu na kukikojolea.

Dr. Ulimboka Anena

Dk Ulimboka aibuka ajipanga kuanika waliomteka
MWENYEKITI wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania,

Dk Steven Ulimboka ameibuka na kusema yuko imara na anajiandaa kuanika
waliomteka, kumtesa na kisha kumtupa katika Msitu wa Pande, nje kidogo
ya Jiji la Dares Salaam.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Dk Ulimbokaalisema kamwe hajanunuliwa
na kwamba ukimya wake wa muda mrefu umetokana na kufuatilia kwa karibu
masharti ya matibabu yake na si vinginevyo.

Rick Ross Ndani Tanzania The Land Of Kilimanjaro

Msanii kutoka Marekani Rick Ross a.k.a the Boss amefika Tanzania kwa
ajili ya Kutumbuisha a.k.a kukamua katika show ya Serengeti Fiesta
2012 ambayo yafanyika katika Viwanja vya Leaders Club hapo kesho
tarehe 6/10/2012. Na amethibitisha kufika kwake kwa kupitia account
yake ya Twitter


Picha: www.shaffihdauda.com

Ajali Jijini Mbeya

Ajali imetokea Jijini Mbeya eneo la Mbalizi na watu kumi wafari na
wengine 25 wajeruhiwa akiwamo mbunge wa viti maalum Mary Mwanjelwa,
ajali hiyo imesababishwa na lori la mafuta lililokata break na kuanza
kugonga magari mengine na mwisho kulipuka. Mungu azilaze mahali pepa
peponi roho za marehemu wote na awaponye majeruhi wote

Ajari Ni Popote

Kweli Ajari ni popote hii ilitokea katika Mto Katuma eneo la Sitalike
Darajani Mkoani Katavi Wilaya ya Mlele, kama Unaingia hifadhi ya Taifa
ya Katavi
Dereva wa gari dogo(pichani) alilielekezea gari mtoni ambako wamejaa
Viboko ili kuepusha kugongana na Lori lililokuwa likipita darajani kwa
wakati huo kutokana na ufinyu wa daraja kutoruhusu gari zaidi ya moja
kupita kwa wakati. Hakuna mtu aliyefariki kulikuwa na majeruhi tu

Auric Air Yaanza Safari za Mpanda

AURIC AIR SERVICES LTD.

ITAFANYA SAFARI ZAKE KATIKA MAENEO HAYA.
NEW SCHEDULE OCTOBER2012. MBEYA: 10 FLIGHTS A WEEK. SONGEA: 5 FLIGHTS
A WEEK. SUMBAWANGA: 3 FLIGHTS A WEEK. MPANDA: 2 FLIGHTS A WEEK.
KIGOMA: 9 FLIGHTS A WEEK. BUKOBA: 9 FLIGHTS A WEEK. IRINGA: 7 FLIGHTS
A WEEK. RUBONDO: 7 FLIGHTSA WEEK. SERENGETI: 7 FLIGHTS A WEEK.

WOTE MNAKARIBISHWA

Mikopo ya Wanafunzi Elimu Ya Juu Wiki hii Kutolewa na HESLB


   Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) itaanza kupeleka fedha za wanafunzi katika vyuo kuanzia wiki hii.
   Ahadi hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, George Nyatega, alipozungumza na NIPASHE.
   Nyatega alisema jumla ya wanafunzi 29,113 wa elimu ya juu nchini kutoka vyou mbalimbali waliochaguliwa kupata mkopo, fedha zao zitaanza kupelekwa kuanzia wiki hii.
   Nyatega alisema baada ya kutoa majina hayo,bodi ya wakurugenzi ilitarajiwa kukutana Jumamosi kufanya tathmini kisha fedha zao zianze kupelekwa vyuoni.
   Hata hivyo alisema kwa mwaka huu idadi ya walioomba mikopo imeongezeka tofauti na mwaka jana na kuongeza kuwa changamoto kubwa inayowakabili ni ufinyu wa bajeti.
   Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Profesa Rwekaza Mukandara, jana aliiambia NIPASHE kuwa chuo hichi kimekubaliana na HESLB kwamba kuanzia Alhamisi wiki hii fedha zitapelekwa.
Chanzo:NIPASHE
chuotanzania.blogspot.com

Shilole Achafua Mashabiki Wake

Hii ndiyo post ya Shilole
Comment ya moja wa mashabiki wake
Jibu alilotoa Shilole
Katika pita pita zangu leo kwenye mitandao ya kijamii leo nimekutana
na kali ya Msanii Shilole kutukana mashabiki wake katika Facebook.
Swali lilibaki kwangu kuwa ile account ya Shilole Facebook ni yake au?
Lakini baada ya mashabiki kumjibu alijaribu juomba ladhi.
Kweli ni Kioo cha jamii????????????

Serengeti Fiesta 2012

Na hatimae Rick Ross kutua Bongo kuja kukamua show ya Fiesta 2012 Dar
es salaam Viwanja vya Leaders tarehe 6 October 2012
Kiingilio: Tsh 20,000 Ukiwahi tiketi yako mapema na Tsh 25,000 Mlangoni
Bhaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaas!

Pamoja FM

Neema yazidi kuufikia mkoa wetu wa Katavi na Sasa Pamoja Fm imeanza
kurusha matangazo yake Rasmi kwa masafa ya fm 98.5 Tune radio Yako
mpaka hapo kwa Wakazi wa Mpanda uweze kusikiliza Radio ya nyumbani.
Kuongezeka kwa Radio ya Tano (5) Pamoja Fm baada ya hapo mwanzo kuwa
na RFA, TBC Taifa, TBC fm na Radio Maria. Sasa kutazidi kufungua
mianya ya uwekezaji na Kufahamika kwa Mkoa mpya wa katavi
Ni Pamoja FM 98.5

Wananchi Wa Rukwa na Katavi Kukutana

Kwa Wale Wananchi wote wenye asili au wanaotokea Mkoa Wa Rukwa na mkoa
Mpya wa Katavi ambao wanaishi Dar na mikoa ya Karibu, Kutakuwa na
mkutano katika Chuo cha Ustawi wa Jamii Dar Es Salaam Ili kupanga
mikakati ya Uzinduzi wa Mkoa mpya wa Katavi. Kikao hicho kitafanyika
siku ya Jumapili tarehe 23/9/2012 Muda ni kuanzia Saa nane mchana
mpaka saa Kumi Jioni
Fika bila kukosa.

TCU yatoa Majina Ya Waliochaguliwa kujiunga na vyuo viwango vyao vya mkopo pamoja na Waliokosa

SELECTED APPLICANTS FOR THE 2012/2013ADMISSIONSThe Tanzania Commission
for Universities(TCU) in Collaboration with the NationalCouncil for
Technical Education (NACTE) isannouncing the names of Applicants who
were seleted into various programs forthe 2012/2013 Admissions.
However, weshall announce the list of  someapplicants who were
selected into variousprograms but obtained no loan,applicants who were
returned by some institutions, and selected applicants whoasked for
transfer, will be announcedbefore 21 September 20121.

1. To view selectedApplicant with no loan/Waliochaguliwa wakakosa
mkopo http://www.tcu.go.tz/uploads/file/SELECTED%20APPLICANTS.pdf

2. To view selected Applicant with loan but subject to verification
with heslb/ Waliochaguliwa wakapata mkopo
http://www.tcu.go.tz/uploads/file/LOANS%20SUBJECT%20TO%20VERIFICATION.pdf

Source: www.heslb.go.tz

Waandishi wa Habari wafanya Maandamano.

Waandishi wa Habari jijini Dar-es-salaam leo wanafanya maandamano
asubuhi hii kuonesha masikitiko yao kwa kuuwawa kwa Mwandishi wa
habari Daudi Mwangosi aliyeuwawa na polisi mjini Iringa

Picha:EARadio

Kifo Cha Mwandishi wa Habari

Vurugu kubwa zilizuka jana katika eneo la Nyororo wilayani Mufindi
kati ya polisi na wafuasi wa Chadema, baada ya askari hao
kusambaratisha mkutano wa chama hicho nakusababisha kifo cha mwandishi
wa habari na watu kadhaa kujeruhiwa.
Mwandishi wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, Daud Mwangosi
anadaiwa kuuawa kwa bomu lililorushwa na polisi katika vurugu hizo.
Awali, inadaiwa kuwa mwandishi huyo alishambuliwa kwa marungu na
Polisi wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), kabla ya bomu hilo
kumjeruhi vibaya tumboni na kusababisha kifo chake.
Mmoja wa mashuhuda wa tukio, alisema wakati mwandishi huyo
akishambuliwa na polisi, mmoja wa askari wa jeshi hilo aliwazuia
wenzake kuendelea kumpiga akiwaeleza kuwa anamfahamu kuwa ni mwandishi
wa habari, huku akimkumbatia.
Shuhuda huyo alidai kwamba jitihada za askari huyo hazikusaidia, kwani
baada ya kutupwa kwa bomu hilo lililosababisha utumbo wa mwandishi
huyo kutoka nje, polisi huyo naye alijeruhiwa mguu.
Hata hivyo, Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Senso alikana polisi
kumuua mwandishi huyo akidai kwamba kilichosababish a kifo chake
nikitu kilichorushwa na wananchi ambapo alisema polisi inakichunguza.
Vurugu hizo ziliibuka baada ya polisi kufika Nyororo na kuwataka
viongozi wa Chadema pamoja na wafuasi wao kutawanyika kwa kuwa
walikuwa hawaruhusiwi kufanya mkusanyiko wowote kutokana na amri
iliyotolewa na jeshi hilo awali.
Polisi mkoani Iringa jana asubuhi walilipiga marufuku kufanyika kwa
maandamano na mikutano yote ya halaiki ya kisiasa mpaka hapo Sensa ya
Watu na Makazi itakapokamilika baada ya kuongezwa wiki zaidi.
Hata hivyo, pamoja na amri hiyo Chadema kilifanya mkutano wilayani
Mufindi kitendo ambacho polisi walisema ni kinyume cha sheria.

Source: Star Tv

Ajari ya Bodaboda agonga(samahani kwa picha)

Dereva bodaboda agonga na kukimbia, ajali hiyo ilitokea maeneo ya
shule ya sekondari Istiquama kijana aliyegongwa alifaliki papo hapo.
Hakika bodaboda zimekuwa chanzo kikubwa cha vifo hapa kwetu.

Ajali Ya Lori.

Ajali ya lori kubwa lilobeba magogo imetokea maeneo ya mgahawa wa
Bismillah karibu na kanisa la Anglican. Taarifa zaidi zitafuata

Picha kwa hisani ya: Majaliwa Rubuye

PICHA ZAIDI KIFO CHA ASKOFU KIKOTI WA JIMBO KUU LA KATOLIKI MPANDA



Makamu wa  Askofu Jimbo Katoriki Mpanda Padre Patrick Kasomo akiwatoa taalifa kwa waumini ya kuwafahamisha kifo cha Askofu wao Paschal Kikoti kilichotokea hapo jana katika Hospitari ya Bugando Jijini Mwanza ambapo mazishi yatafanyika siku ya juma mosi wiki hii ndani ya Kanisa la Parokia kuu Jimbo la Mpanda.
 Waumini wa Kanisa Katoriki Jimbo la Mpanda wakimlilia Askofu wao Paschal Kikoti mara baada ya kutangaziwa na makamu wa Askofu wa Jimbo la Mpanda Padri Patrick Kasomo kuwa Askofu Paschal Kikoti amefariki majira ya saa 2:30 usiku katika Hospitari ya Bugando hapo jana. Picha na Walter Mguluchuma Katavi Yetu.
Blogzamikoa
Chanzo: kataviyetu.blogspot.com