WAJUMBE WA UKAWA WATINGA BUNGENI

Katibu wa Bunge Maalum la Katiba Yahya Khamis Hamad Amethibitisha kuwepo kwa wajumbe wa Bunge hilo kutoka kundi la Ukawa ambao wanashiriki vikao na wengi wamejisajili lakini hawajashiri kikatika kamati yoyote.

Amesema katika uchunguzi alioufanya wajumbe waliojisajili na kutoshiriki vikaoni pamoja na Leticia Nyerere, Clara Mwituka Pamoja na John Shibuda wote kutoka chadema.

Aidha amewataja wajumbe wengine kutoka Ukawa ambao wanashiriki vikao ni pamoja na Fatuma Ally, Jamila Abed na Omary Alyla Katiba kamati namba 2 wanasema majadiliano yanaendelea vizuri licha ya kuwepo na changamoto mbalimbali Miongoni mwa wajumbe Kutoka ukawa walionekana Mjini Dodoma ni pamoja na Chiku Abwao ambaye anasema amekuja kwa kazi zake binafsi na kamwe hawezi kushiriki vikao hivyo.

Shamsi Vuai Nahodhani mwenyekiti kamati namba 3 na Dk Francis Michael ni mwenyekiti kamati namba mbili wanasema kwasasa tayari wamekwisha anza kujadili sura ya 3,4,5 na tano,licha ya changamoto mbalimbali zinazojitokeza.

Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba wameanza kukaa kwenye kamati katika kumbi mbalimbali zilizopo Mkoani humo tarehe 6 mwezi huu kwaajili ya kujadili sura 15 za Rasimu ya Katiba zilizokuwa zimeb aki na kazi hiyo itafanyika kwa siku 15, ambapo watarejea tena ndani ya bunge.