SUNGUSUNGU WAFANYA MAUAJI

Mauaji ya kutisha ya watu wawili yanadaiwa kufanywa na kundi la Askari wa jadi maarufu kama Sungusungu wilayani Manyoni mkoani Singida baada ya kuwatoa nyumbani kwao usiku na kuwapeleka kichakani ambako waliwashambulia kwa kipigo kisha kumchoma moto mmoja akiwa mfu na mwingine akiwa bado hajakata roho.

Marehemu hao wanajulikana kwa majina ya Lameck Joshua (31) na Doto Kindai ( 20), na taarifa zilizozagaa kijijini hapo ni kuwa watu hao wameuawa kikatili kwa madai kuwa ni weziwa mifugo hata hivyo serikali ya kijji haina taarifa za watu hao kujihusisha na vitendo vya wizi.