WAKRISTO WATOROKA MJI WA QARAQOSH IRAQ

Maelfu ya Wakristu wanatorokea maisha yao katika mkoa wa Nineva baada ya wapiganaji wakiislamu waThe Islamic State kuuteka mji wa Qaraqosh.

Afisa wa ngazi ya juu wa Kikurdi kaskazini mwa Iraq ameonya kuwa watu 50,000 wa jamii ya Yazidi watakabiliwa na njaa ikiwa hawatapata msaada wa dharura.

Jamii ya Yazidi ilikimbilia maeneo ya milima ikiwa na chakula kidogo na maji baadaya wapiganaji wa jihad kutoka kwa kundi la Islamic State kuvamia mji wa Sinjar mwishoni mwa wiki.

Wapiganaji wa Kikurdi Peshmerga awali wakidhibiti mji huo wa Mosul.

Jabbar Yawar, ambaye ni kiongonzi wa wapiganaji wa kikurdi anasema kuwa tayari wengi wao wameaga dunia

Kutekwa kwa mji wa Qaraqosh kumesababisha kukimbia kwa maelfu ya watukaskazini mwa Iraq kutokana na vitishovya makundi ya Jihad.

Kushindwa kwa vikosi vya kikurdi kudhibiti mji huo na mji mingine kutoka kwa mikono ya wapiganaji wa Islamic State kutasabaisha mengi..

Wapiganaji wa Kikurdi wa Peshmerga walikimbia mji huo bila kupingwa.

Kasisi mmoja mkuu wa eneo hilo ameliambia shirika la Habari la Ufaransa kuwa, maelfu ya watu wanaonekana wakikimbia kwa hofu.

Kuondoka kwa watu hao kunafutia kuondoka kwa wakrito wengine kutoka mji wa Mosul baada ya kuamrishwa kundoka , kubadili dini au kuawa na wapiganaji wa Jihad.

Wapiganaji wa The Islamic State wameteka kiasi kikubwa tu cha ardhi kutoka Iraq na Syria ambayo wametangaza kuwa taifa la kiislamu.

Inakisiwa kuwa wakaazi laki moja wameshatorokea maeneo ya Kurdistan.