MABASI YAGONGANA USO KWA USO, YAUA NA KUJERUHI

Hali ni tete sana eneo la Mkolye, takribani km 4 toka Mjini Sikonge baada ya basi la Sabena toka Mbeya kwenda Mwanza na basi la A.M. toka Tabora kwenda Katavi kugongana uso kwa uso (head on collision).

Dereva wote wa mabasi hayo wamefariki hapo hapo, mmoja akiwa amekatika kichwa!
Nimeshuhudia abiria kadhaa wakiwa wamenasa katika mabasi hayo, baadhi wakiwa wamekatika mikono na miguu!

Abiria wapatao 18 wamefariki mpaka sasa na majeruhi zaidi ya 30 wamepelekwa katika Hospitali ya Mission ya wilayani Sikonge.

Chanzo cha ajari ni dereva wa basi la Sabena kutoka Mbeya kwenda Tabora kutaka kuovertake gari ambapo vumbi lililokuwa limetimka lilifanya ashindwe kuona na kusababisha kukumbana uso kwa uso na basi A.M kutoka Mwanza kuja Katavi

Neno langu: SUMATRA wanatakiwa kusimamia hii njia ya Mwanza-Tabora-Katavi kwa mwendo mabasi yanaoutumia ni wa hovyo na kasi sana. Mungu azilaze mahara pema peponi roho za marehemu na awatie nguvu wafiwa, Awaponye wale majeruhi wote