BABA AWACHOMA WANAE MOTO KISA KUANGALIA TV KWA JIRANI

Salum Juma, fundi gereji wilayani Temeke, mkazi wa Mbagala Kibonde Maji, jijini Dar es Salaam anadaiwa kuwachoma moto mikono watoto wake wawili kwa kutumia tambi za jiko kisa ni kuangalia TV kwa jirani.

Watoto hao, Agustino Said (7), mwanawe wa kufikia na NurdinSaid (5), wa kumzaa mwenyewe, walikutwa na mkasa huo baada ya kwenda kuangalia runinga kwa jirani na kurudi nyumbani saa 5:00 usiku

Kitendo hicho kilifanyika huku mama yao akiwa kwenye biashara zake za kukaanga mihogo.