WANAOFUGA NDEVU NA KUVAA HIJAB MARUFUKU CHINA

Wanaume wanaofuga ndevu pia wameambiwa wasipande kwenye usafiri wa umma.

Mji mmoja wa China wa mkoa wa Xinjing umekataza wale wote wanaovaa nikab na kufuga ndevu kupanda kwenye usafiri wa umma, limeeleza gazeti moja nchini humo.

Maafisa wa Karamay walisema katazo hilo, ambalo linakataza uvaaji wa hijab, nikab na burka kuwa utaisha Agosti 20 kutokana na matukio ya michezo.

Xinjiang, ni makazi yenye Waislamu wa Uighur wachache, umekumbwa na ghasia miezi ya karibuni.

Wanawake wanaovaa nikab, hijab na burka wamekatazwa kupanda usafiri wa umma katika jimbo hilo.Uongozi umeilamu Uighur wanaotaka kujitenga kwa kufanya ghasia hizo.

Katika ripoti iliyotolewa na gazeti la Karamay Daily ambalo huendeshwa na chombo cha habari cha taifa hilo, maafisa hao walitaja "watu wa aina tano" ambao wamekatazwa kupanda usafiri wa umma.