RAGE, TAMBWE WAPATA AJALI

WABUNGE Wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wamelazwa katika Hospitali ya Mkoa wa Dodoma baada ya gari walilokuwa wakisafiria kutoka Tabora kwenda Dodoma kuhudhuria vikao vya Bunge Maalum la Katiba kupata ajali.

Wabunge hao ni Mbunge wa Tabora Mjini, Aden Rage na Mbunge wa Viti Maalum, Munde Tambwe. Majeruhi wengine katika ajali hiyo ni Issa Chimwaga (31), Mwanahamisi Ramadhani (34), John Hoya (32) ambaye ni dereva ambapo pia hakuumia katika ajali hiyo.

Kwa mujibu wa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Dodoma, Dk Ezekiel Mpuya alisema jana mchana walipokea majeruhi wannewa ajali hiyo wakiwemo Wabunge Rage na Munde.

Alisema majeruhi hao walitokana na ajali waliyoipata katika eneo la Chigongwe Manispaa ya Dodoma walipokuwa wakisafiri kwenda Dodoma kwa gari binafsi.

Dk Mpuya alisema vipimo vimeonesha Munde pamoja na kupata majeraha usoni na kichwanipia amevunjika mkono wakati Rageameteguka bega la kushoto. Hata hivyo, alisema hali zao zinaendelea vizuri na wanaendelea na matibabu.

Hata hivyo, Rage na Munde wamelazwa katika Wodi namba 18 Grade One chumba namba moja na mbili wakiwa na majeraha mbalimbali mwilini. Akizungumza akiwa wodini Rage alisema amepata majeraha katika bega la kushoto na eneo la nyuma ya mgongo.

Alisema ajali hiyo ilitokea baada yadereva wa gari lao anataka kulipita lori lakini ghafla dereva wa lori hilo akaingia katikati ya barabara.

Alisema dereva wao alipoona hivyo badala ya kuligonga lori aliamua kwenda pembeni ndipo gari lao likaruka na kuingia kwenyekorongo na kupinduka.

Alisema kilichowasaidia walikuwa wamefunga mikanda jambo ambalo. Kwa upande wake Tambwe alikuwa akilalamikia maumivu katika sehemu za kichwani na mkono.

Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Usalama barabarani Mkoa wa Dodoma, Peter Sima alipotakiwa kuzungumzia ajali hiyo alisema bado anakusanya taarifa na kuahidi kutoa taarifa baadaye.

Hata hivyo, taarifa kutoka kwa ndugu wa karibu wa familia za wabunge hao iliyopatikana baadaye jana, ilisema wabunge hao walichukuliwa kwa ndege maalumu jana jioni kupelekwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Dar kwa matibabu zaidi.