URUSI YALIPIZA KISASI MAREKANI NA ULAYA

Urusi imetangaza marufuku ya vyakula kutoka kwa muungano wa Ulaya, Marekani na nchi zingine kadha za magharibi ambazo zilikuwa zimetangaza vikwazodhidi ya Urusi kutokana na sera zake nchini Ukraine.

Waziri mkuu nchini Urusi Dmitry Medvedev aliuambia mkutano wa serikali kuwa Urusi haitaruhusu tena uingizwaji wa Nyama, Samaki, Matunda na bidhaa zingine kutoka mwa jumuiya ya Ulaya, Marekani, Australia,Canada na Norway.

Medvedev amesema kuwa vikwazo hivyo vitadumu kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Amesema kuwa Urusi inatathmini kupiga marufu mashirika ya ndege ya nchi za magharibi yanayotumia anga ya Urusi kuingia barani Asia.

Wadadisi wanasema kuwa Urusi inategemea zaidi chakula kutoka nje asilimia kubwa ikiwa ni kutoka kwa nchi za magharibi.