BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI(HESLB) YATOA MAJINA YA WANAFUNZI AMBAO HAWAJAKAMILISHA BAADHI YA TAARIFA

Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu(HESLB) katika mchakato wa kuhakikisha taarifa za wanafunzi walioomba mikopo katika mwaka wa masomo 2014/2015 wamegundua baadhi ya makosa katika form za waombaji, Hivyo wametoa majina ya wanafunzi wote walioomba mikopo kwa mwaka wa masomo 2014/2015 ambao hawaja kamilisha baadhi ya taarifa.

Wanafunzi ambao hawaja ambatanisha baadhi ya taarifa kama vyeti vya kuzaliwa, Picha(passport size), nakala za kitambulisho cha mpiga kura au pasi ya kusafiria wanatakiwa kutuma taarifa zao kwa The Executive Director, Higher Education Students' Loans Board, P. O. Box 76068,DAR ES SALAAM. Kwa kuambatanisha na barua ambayo itakuwa na Majina Kamili pamoja na Namba ya mtihani wa kidato cha nne(form four)

Kwa wale ambao hawajaweka sahihi ya muombaji (Applicant signature) na sahih ya mdhaming wanatakiwa kufika makao makuu ya bodi ya mikopo HESLB offices on Plot No. 8, Block No. 46 Sam Nujoma Road, Mwenge- Dar es Salaam wao wenyewe nasi mwakilishi wao.

Ili kuangalia majina ya waombaji ambao taarifa hii inawahusu watembelee link ifuatayo:-

http://www.heslb.go.tz/index.php/application-guidelines/168-call-for-loans-applicants-to-correct-their-loan-applications ??