''UKAWA WAMEPOTOSHA'' JK

RAIS Jakaya Kikwete amewataka wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, waliojiundia kundi la Umojawa Katiba ya Wananchi (UKAWA), warudi katika Bunge hilo, watumie mifumo maalumu waliyojiwekea na kanuni walizojitungia wenyewe, kutafuta maridhiano.

Ametoa kauli hiyo jijini Dar es Salaam jana wakati wa hotuba yakealiyoitoa kwa Taifa katika utaratibu aliojiwekea wa kuzungumza na wananchi kila mwisho wa mwezi.


Rais Kikwete amewataka wajumbe hao, watafute maridhiano kwa kutumia mifumo hiyo rasmi, na yeye yupo tayari kusaidia pale watakapohitaji msaada wake kuhusu suala hilo, ili Watanzania wapate Katiba bora wanayoihitaji.Ameonya kuwa ikiwa maridhiano wanatafuta nje ya mifumo hiyo, watakuwa wakitumia mitandao tu isiyokuwa na faida kwao wala jamii.

Mbali na kuwapa onyo hilo, pia aliwakumbusha kuwa Bunge Maalumu la Katiba lina mamlaka ya kutunga Katiba, na kama isingekuwa hivyo kusingekuwa na haja ya kuwa na siku 70 za awali nayeye kupewa mamlaka ya kuongeza siku 60 kujadili.

Alionesha kuwashangaa wajumbe hao kwamba, kanuni na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba waliitunga wenyewe na sasa katika utekelezajiwa sheria hiyo, wanasusia vikao jambo alilosema si haki kwa ummawa Watanzania.

Kikwete alisema yeye si Mwanasheria hivyo anakiri kwamba anaweza kuwa na upungufu katika kuelewa maana yabaadhi ya maneno ya kisheria, lakini akasema hakumbuki kuwepokwa kifungu chochote katika Sheria, kinachosema kuwa Bunge Maalumu la Katiba halina mamlakahayo.

"Tangu tuliposikia maneno hayo yakisemwa (kwa Bunge Maalumu haliwezi kubadilisha rasimu ya Katiba), nimeuliza nithibitishiwe ukweli wa madai hayo lakini bado sijaambiwa vinginevyo. Kama ukweli huo upo naomba wanisaidie," alisema Rais Kikwete.

Alisema badala yake ameambiwa kuwa maneno yaliyotumika katika Sheria, hayaakisi dhana inayotolewa kuwa kazi ya Bunge Maalumu la Katiba ni kubariki Rasimu na si kufanya vinginevyo."Nimeambiwa kuwa sheria inasema Tume itaandaa Rasimu ya Katiba na Bunge Maalumu la Katibalitatunga Katiba iliyopendekezwa," alifafanua Kikwete.

Akielezea hatua iliyofikiwa kabla yakuahirishwa kwa Bunge hilo Aprili 25 mwaka huu kupisha Bunge la Bajeti na Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Rais Kikwete alisema wakati baadhi ya wajumbe wa vyama vya Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi, wakisusia vikao Aprili 16, kazi kubwa ilikuwa imefanyika."Tayari kamati zote 12 za Bunge hilo zilikuwa zimekamilisha kujadiliSura ya Kwanza na ya Sita za Rasimu ya Tume. Sura hizo zinazungumzia utambulisho wa nchi na muundo wa Muungano.

"Kamati zote zilipiga kura ya kupitisha uamuzi wao kuhusu sura hizo mbili. Kamati kadhaa ziliweza kupata theluthi mbili ya kura kwa wajumbe wa pande zote mbili za Muungano, jambo lililoonesha dalili njema kwamba Katiba mpya inaweza kupatikana," alisisitiza Kikwete.Alisema kazi iliyobaki baada ya taarifa ya kila Kamati kuwasilishwa kwenye Bunge zima, ni Kamati ya Uandishi kukamilisha taarifa yake na kuiwasilisha kwenye Bunge zima kwa ajili ya kujadiliwa.

Alisema ikijadiliwa wajumbe watapiga kura kuamua kuhusu Sura hizo mbili kwa kutumia theluthi mbili ya kura za kila upande wa Muungano.

Kuhusu Ukawa kususia vikao vya Bunge hilo, Rais Kikwete alisema sababu walizotoa zimekuwa zikiongezeka na kubadilika kadri siku zinavyosonga mbele na upepowa kisiasa unavyokwenda.

"Hivi sasa wanazungumzia mambo mawili. Kwanza, kwamba Bunge Maalumu halina mamlaka ya kuifanyia mabadiliko yoyote Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa naTume ya Mabadiliko ya Katiba. Kwa maoni yao, kazi ya Bunge Maalumu la Katiba ni kujadili na kupitisha tu Rasimu ya Katiba ya Tume na siyo kubadili chochote.
Pili, wametoa sharti la wao kurudi bungeni ni kuhakikishiwa kwamba, kitakachojadiliwa bungeni ni Rasimu ya Tume. Bila ya sharti hilokukubaliwa, wamesisitiza kutorudi bungeni," alieleza Kikwete.

Akifafanua suala hilo, Kikwete ambaye alihusika kubuni wazo la kuwa na mchakato wa kuandika Katiba mpya, na katika maandalizi ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, ya kuongoza na kuendesha mchakato huo, alisema hakuna popote katika vikao vya Baraza la Mawaziri kujadili Rasimu ya Muswada wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba walipozungumzia Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, kuwa haiwezi kufanyiwa marekebisho na Bunge Maalumu la Katiba.

Alisema ndio maana suala hilo limewekwa kisheria kwa uwakilishi mpana kupitia ngazi nne muhimu za mchakato wa kutunga Katiba hiyo ikiwamo wananchi kutoa maoni, Mabaraza ya Katiba ya Wilaya na Mabaraza ya Kitaasisi kutoa maoni yao kuhusu Rasimu yakwanza ya Katiba iliyotayarishwa naTume.

Bunge Maalumu na Kura ya Maoni itakayoshirikisha wananchi wote ambao ndio wenye kauli ya mwisho kuhusu Katiba wanayoitaka.

Alisema mamlaka ya kutunga Katiba kwa mila na desturi za mabaraza ya kutunga sheria, ni uwezo wa kurekebisha, kubadili, kufuta na hata kuongeza kilichopendekezwa. Alisema kama ingekuwa kilichokusudiwa ni kubariki tu, kusingekuwa na haja yaneno "kutunga Katiba" wala kura inayohitaji theluthi mbili.

Kikwete alisema anapata shida kuelewa mkanganyiko unatokea wapi kutokana na ukweli kwamba wale wanaoongoza kuhoji mamlakaya Bunge Maalumu, ni wale wale waliotunga Sheria ya Mabadiliko yaKatiba tena hatua kwa hatua.

Alisema siku zote za mjadala kilichokuwa kikijadiliwa ni Sura ya Kwanza na Sura ya Sita hivyo haiingii akilini kudai kuwa kinachojadiliwa bungeni humo si Rasimu ya Katiba iliyowasilishwa na Tume ya Jaji Warioba.

Aliwataka Ukawa kuwa wakweli kwaWatanzania na kueleza kabla huenda katika Kamati kumefanyikamarekebisho kwenye Rasimu ambayo hayakuwapendeza kuliko kusema mambo yasiyowakilisha ukweli halisi wa Rasimu inayojadiliwa na kuwafanya watu waamini kinachojadiliwa si rasimu hiyo ya Jaji Warioba na kwamba ni matakwa ya CCM.

Kikwete alisema kama Ukawa hawakuridhishwa na yaliofanyika, walipaswa kutumia mifumo waliyojitengenezea wenyewe kwenye Kanuni kumaliza tofauti zao.

"Kanuni zinaelekeza kuwa mambo wasiyoridhika nayo yajadiliwe kwenye Kamati ya Mashauriano na Maridhiano. Ukiacha mifumo ya maridhiano ndani ya Bunge ukaenda nje kwa wananchi au vyombo vya habari na mitandao si jawabu la tatizo," alisema Kikwete.Aliwasihi Ukawa warejee bungeni na watumie mifumo maalumu ya Bunge iliyowekwa na Kanuni kutafuta maridhiano na wasichoke kuwa na mawasiliano na vyama vingine vya siasa na hasa CCM kutafuta maelewano.

"Mimi niko tayari kusaidia pale watakapoona inafaa kufanya hivyo kama ambavyo nimekuwa nikifanya siku za nyuma," alisema Kikwete.Alisisitiza kuwa ili kupata Katiba mpya inayohitajika, maelewano baina ya wadau wakuu wa kisiasa nijambo lisilokuwa na badala yake. Vinginevyo kupata theluthi mbili kwa pande zote mbili za Muunganohaitawezekana.Alimpongeza Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi, kwa uamuzi wa kuvikutanisha vyama vinne vikuu vya siasa kujadili suala hilo.

"Ombi langu kwa viongozi wa vyama hivyo ni kuitumia vyema fursa ya majadiliano kuukwamua mchakato kwa maslahi ya nchi yetuna watu wake," alisisitiza Kikwete na kumpongeza Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta kwa juhudi za kusaka maridhiano ingawa wajumbe waliosusia vikao hawakushiriki, alimtaka asikate tamaa.Kikwete alisema amesikia madai kwamba hotuba yake ya ufunguzi ndio iliharibu mchakato na kwamba ameikana Rasimu ya Katiba ambayo na yeye ni mmoja wa watu waliotia saini.

Nadhani ndugu zetu wanaotoa madai haya wameitafsiri isivyo, saini yangu katika Gazeti la Serikali lililotangaza rasmi Rasimu ya Katiba na Taarifa ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba.

Alisema katika kutangaza katika Gazeti la Serikali sharti linamtaka anayetangaza ajitambulishe kuwa yeye ni nani na atie saini yake. Kwa kufanya hivyo, hakumfanyi yeye kuwa naye ni mhusika na maudhui ya kila kinachopendekezwa na Tume.Jambo lingine linalofanana na hilo ni yale madai kwamba nilikuwa napata taarifa ya maendeleo ya mchakato ndani ya Tume mara kwamara, iweje leo nitoe maoni tofauti kama niliyoyatoa katika hotuba yangu kwenye Bunge Maalumu.

Ni kweli kabisa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Mheshimiwa Jaji Joseph Warioba, Makamu wake, Mheshimiwa Jaji Agustino Ramadhani na Mheshimiwa Dk Salim Ahmed Salim wamekutana na mimi kwa nyakati mbalimbali kuzungumzia mwenendo wa mchakato. Lakini, hayakuwa mazungumzo ya kina kuhusu nini kiwe vipi katika maudhui na mapendekezo ya Tume, alieleza Kikwete.

Alisema Rasimu zote mbili nilizipata mara ya kwanza alipokabidhiwa rasmi, tena kwa uwazi na kwamba watu wasijenge dhana kuwa alipewa Rasimu na kuisoma kabla ya kukamilika na hivyo nilitoa maoni yake Tume hii ilikuwa huru na niliiacha iwe hivyo.

Sikuiingilia kwanamna yoyote ile kupenyeza mambo ninayotaka yawemo. Kuthibitisha dhamira yangu ya kutaka Tume iwe huru katika kufanya kazi zao hata pale waliponitaka nitoe maoni niliwaomba tusifanye hivyo ili nisiwakwaze katika kufanya kazi zao, wakapata taabu ya kuwianisha wanayofikiria na mawazo yangu, alisema Kikwete. Kuhusu hotuba yake kuvuruga mchakato, Kikwete alisema madai hayana ukweli wo wote wala msingi kwani hakuna chaajabu alichofanya siku alipohutubiaBunge hilo.

Ukweli ni kwamba nilisema yale yale ambayo Tume yenyewe imeyasema katika Rasimu ya Katiba na Taarifa za Tume.

Niliyoyasema kuhusu malalamiko ya watu wa pande zetu za Muungano na uzuri na changamotoza miundo ya serikali mbili na serikali tatu ni yale yale yaliyomo kwenye taarifa za Tume.

Nimetumia takwimu zile zile za Tume.

Pengine kilichoonekana kuwa kibaya ni jinsi nilivyozifasiri taarifa hizo na mapendekezo ya Tume, alisema Kikwete.Alisema haoni kosa lake kutoa maoni kuhusu baadhi ya vipengele vya Rasimu hususan uandishi na dhana mbalimbali zilizokuwamo kwa kuwa ilitolewa hadharani ili ijadiliwe.

Lakini, pia mimi ndiye Rais wa nchi yetu, ninayo dhamana ya uongozi na ulezi wa taifa letu. Itakuwaje kwa jambo kubwa la hatma ya nchi yetu nilinyamazie kimya. Watanzania wangeshangaa na wangekuwa na haki ya kuhoji Rais wao ana maoni gani. Bahati nzuri nilitoa maoni yangu mahali penyewe hasa, na kwa uwazi, kwenye Bunge Maalumu la Katiba.Hata hivyo, ni muhimu kusisitiza kuwa namna nilivyotoa maoni yangu sikuwa natoa maagizo wala kushurutisha, ndiyo maana kila wakati niliwakumbusha Wajumbe kuwa mamlaka ya uamuzi ni yao.

Yangu yalikuwa maoni tu wanahiariya kuyakubali au kuyakataa, alisema Kikwete.Kuhusu muundo wa serikali tatu, nilieleza wazi kuwa sina tatizo nao kama ndiyo matakwa ya Watanzania. Lakini, nilieleza hofu yangu kuhusu mapendekezo ya Tume na kuwataka Wajumbe wafanye kazi ya ziada kuondosha udhaifu iwapo wataukubali muundo unaopendekezwa.

Nilieleza nia yangu ya kutaka tuwe na Serikali ya Muungano yenye ukuu unaoonekana, yenye nguvu ya kuweza kusimama yenyewe, inayoweza kuwa tegemeo kwa nchiwashirika, Serikali isiyokuwa tegemezi wala egemezi kwa nchi washirika na ambayo inavyo vyanzo vya uhakika vya mapato.

Hivi kwa kutoa ushauri huo kwa Wajumbe wa Bunge Maalumu la Katiba inageuka kuwa nongwa. Kwakweli sielewi lawama ni ya nini, alibainisha Rais. Alisema anachoamini hastahili lawama bali pongezi kwa kuwa muwazi na kutoaushauri wa msingi ambao utasaidianchi kupata Katiba nzuri inayojali maslahi ya watu wa nchi yetu na yanchi zetu mbili zilizoungana miaka 50 iliyopita.

Rais alitaka mgogoro uliopo sasa katika mchakato wa Katiba usiendelee kwani malalamiko ya wajumbe wa Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi yanaweza kushughulikiwa kwa ukamilifu katika mifumo ya Bunge hilo. Nawasihi waitumie. Hali kadhalika, kwa kupitia mazungumzo wanayofanya na wenzao wa CCM wanaweza kutengeneza nguvu ya pamoja kutatua changamoto za sasa na zitakazojitokeza baadaye.

Kilicho muhimu ni kwa pande zote kuwa na dhamira ya dhati ya kutoka hapa tulipo sasa. Kama utashi wa kisiasa upo kwa kila mmoja wetu, hilo ni jambo linalowezekana kabisa. Narudia kuahidi utayari wangu wa kusaidia kadri inavyowezekana tusonge mbele, alihitimisha Rais Kikwete.