POLISI WAMKAMATA MPIGA RISASI WANAWAKE ARUSHA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha Liberatus Sabas amesema jeshi hilo linamshikilia mtuhumiwa wa matukio ya kuwapiga risasi wanawake jijini Arusha.

Mtu huyo ni Adam Mussa, mwenye umuri wa miaka 30, mkazi wa Majengo Jijini Arusha ambaye amekamatwa na bastola mbili zikiwa na risasi kumi.

Akiongea na waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda Liberatus Sabas amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa Agosti26 mwaka huu, majira ya usiku, nyumbani kwake Majengo Juu.

Kamanda Sabas amesema baada ya kumkamata mtuhumiwa na kumhojiambapo alikiri kuhusika katika matukio yanayoendelea jijini Arusha ya upigaji wanawake risasi na moja kati ya silaha hizo iliibiwa ndani ya gari la mfanyabiashara Seleman Bakari Msuya mkazi wa Sombetini, baada ya watu wasiojulikana kuvunja kioo cha gari na kuichukua.

Mtuhumiwa anatarakiwa kufikishwa mahakamani mara baada ya upelelezi kumalizika.

Kamanda Sabas ametoa wito kwa wananchi kuendelea kutoa siri za mtandao huo uliozuka ghafla mwezo Agosti mwaka huu na kujeruhi na kuua wanawake wenye magari mjini Arusha, ambapo hadi sasa tayari watu nane wanashikiliwa kwa kuhusiana na matukio hayo.