GENERAL AL-SISI APANDISHWA CHEO NA KUWA FIELD MARSHALL

Kaimu Rais wa Misri Adly Mansour ametangaza kwamba mkuu wa jeshi ambae pia ni Waziri wa ulinzi, Generali Abdel Fattah Al-Sisi amepadishwa ngazi na kua Field Marshall{Cheo cha juu zaidi katika Jeshi).

Kuna minong'ono kwamba huenda Generali Al Sisi akawania Urais wa Misri katika miezi michache ijayo.

Anaaminika kuchangia pakubwa katika kumuondoa madarakani Rais aliyeegemea misingi ya kiisilamu Mohammed Morsi mwaka jana kufuatia maandamano makubwa dhidi yake.

Abdel Fattah al-Sisi, anaonekana kupendwa sana kiasi kinachofananishwa tu na alivyopendwa Gamal Abdel Nasser lakini baadhi wanahisi kuwa kutawala kwake kunaweza kurejesha hali ya ukandamizaji ulioshudiwa chini ya utawala wa Hosni Mubarak.