RWANDA YAKOSOLEWA KWA KUKANDAMIZA UPINZANI

Afisaa mmoja mkuu katika Umoja wa mataifa, amekosoa ambavyo serikali ya Rwanda inawatendea wanasiasa wa upinzani.

Akiongea na BBC, wiki moja baada ya ziara yake nchini humo, mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa, Maina Kiai alisema kuwa karibu kila mwanasiasa, anayejitokeza hadharani kupinga serikali, huishia kwenye matatizo ya kisheria.

Baadhi hukamatwa na kufungwa jela kwa kile kinachosemekana kuwa kueneza uvumi.

Bwana Kiai alisema kwamba alizungumza na mwanamume mmoja akiwa gerezani kuhusu siasa.

Kiai amesema kuwa angali anafanya mazungumzo ya kina naserikali ya Rwanda kuhusu hilo