MAUWAJI YA KINYAMA YAKITHIRI MUSOMA

Vitendo vya Mauaji ya watu katika maeneo mbali mbali vimeanza kujitokeza katika wilayani za Butiama na Musoma Mjini Mkoani Mara, kufuatia watu wawili Kuwawa akiwemo mama mmoja Mkaguru Magee mkazi wa kijiji cha Mkirira na Mzee Aitwaye Shaabani Mkazi Nyakato katika wa manspaa ya mji wa Musoma kuuwawa kikatili na watu wasiojulika.

Wakiongea kwa Nyakati Tofauti Mashuhuda wa matukio hayo wanasema kuwa matukio kama haya yalijitokeza mwaka jana kwa kuuwawa kwa wanawake na wazeezaidi ya 17 katika wilaya hizo kwa kuchinjwa jambo lililowatia hofu na kuiomba Serikali kusaidia kupambana na tatizo hilo kutokana na matukio hayo kuanza tena kujitokeza na kuwafanya washindwe kufanya shughuli zao za kifamilia kwa kuhofia maisha yao.

Ni miongoni mwa akinamama wakazi wa Wilaya za Butiama na Manspaa ya Mji wa Musoma, wakionyesha majonzi yao kufuatiavifo vya mfululizo vya Watu wawili waliouwawa kikatili na watu wasiojulikana na miili yao kutelekzwa katika kijiji cha Mkirilana kiongoji cha msikamano eneo la Nyakato mjini Musoma.


Wakizungumza viongozi wa Serikali ya Kijiji cha Mkirila na mwenyekiti wa kitongoji cha Mshikamano mjini Musoma wameonyesha kukata tamaa kutokana na kukithili kwa matukioya mauaji katika maeneo hayo.

Kwa upande wa viongozi mbali mbali wanasema kuwa matukio yamauaji katika maeneo hayo yanatokana na wakazi wake kushindwa kutoa ushirikiano kwa jeshi la Polis ili kuwashughulikia watuhumiwa.

Nae mwenyekiti wa kamati ya Urinzi na usalama wa wilaya ya Butiama mama Anjerina Mabula,anatoa kauli ya Serikali katika kupambana na matukio hayo.