JARIBIO LA KUMUUWA WAZIRI LAGUTUKIWA

Kumekuwa na jaribio lililotibuka la kumuua kaimu waziri wa ndani nchini Libya Al-Sidik Abdel-Karim.

Shirika la kitaifa la habari LANA na lile la AFP yamethibitisha tukio. Inaarifiwa kwamba gari alimokuwa Abdel Karim lilipigwa risasi alipokuwa akielekea katika mkutano katika makao makuu ya bunge.

Abdel-Karim anatarajiwa kuhutubia waandishi habari hivi punde.

Abdel Karim aliteuliwa na waziri mkuu nchini Libya kuwa kaimu waziri wa ndani baada ya waziri Mohamed Sheikh kujiuzulu mnamo Agosti mwaka jana.

Seddik Abdelkarim, alikuwa katika gari lake aliposhambuliwa na watu wasiojulikana waliomfyatulia risasi.

Inaarifiwa hakuna aliyeuawa kwenye shambulizi hilo.

Libya imekuwa ikikabiliwa na halingumu ya kisiasa tangu waasi kuipindua serikali na kumuua aliyekuwa Rais Muamer Kadhafi mwaka 2011.

Waziri huyo alikuwa njiani kuelekea bungeni wakati gari lake liliposhambuliwa.

Shambulizi lenyewe limetokea chini ya wiki tatu baada ya mauajiya naibu waziri wa viwanda Hassan al-Droui, aliyeuawa mjini Sirte.