NDEGE ISIYO NA RUBANI(DRONE) YATUMIKA KUSIMAMIA MTIHANI

Ndege isiyo na rubani (drone) yatumika kusimamia mitihani.

Shule moja ya nchi Ubelgiji imeamua kutumia ndege isiyo na rubani (drone) kusimamia mitihani baada ya kushindwa mbinu za kawaida kuwazuia wanafunzi kufanya udanganyifu katika mitihani yao.

Ndege hiyo ina kamera ya kuchukua picha za video pamoja na kurekodi harakati yoyote inayotia wasiwasi kutoka kwa mwanafunzi yeyoteyule na kurusha moja kwa moja kwenye TV harakati yoyote ile isiyo ya kawaida.