REAL MADRID KLABU TAJIRI ZAIDI, MAN U CHALI

Klabu ya Real Madrid imehifadhi taji la kuwa klabu tajiri zaidi duniani kwa msimu wa tisa mfululizo, kuambatana na orodhaya vilabu tajiri iliyochapishwa na kampuni ya uhasibu ya Deloitte.

Klabu nyingine ya Uhispania, Barcelona inashilikia nafasi ya piliikifuatwa na Bayern Munich ya Ujerumani, katika nafasi ya pili na tatu mtawalia.

Kwa mara ya kwanza klabu ya Manchester United ambayo kwa sasa imekabiliwa na msururu wa matokea mabaya katika ligi kuu ya Premier ya England, imeshushwa miongoni mwa vilabu tatu tajiri zaidi duniani kwamara ya kwanza kwa zaidi ya miaka kumi na saba iliyopita.

Manchester city imepanda mpaka nafasi ya sita kuzipiku Chelsea(7), na Arsenal(8)

Waandishi wa habari wanasema kuwa ligi ya vilabu vingi kuzalisha kiasi kikubwa cha fedha, nyingi yavilabu hivyo vinaendelea kupata hasara kubwa kutokana na gharama za mishahara na malipo ya usajili wa wachezaji.