LIGI YA MKOA WA KATAVI YAANZA KUTIMUA VUMBI

Mashindano ya Ligi ya Taifa ngazi ya Mkoa katika mkoa wa Katavi yameanza kutimua vumbi katika uwanja wa Azimio uliopo Mjini Mpanda.

Mashinano hayo yanayoshirikisha timu tisa yameanza jana ambapo timu zimepangwa katika makundi mawili.

Kundi A lina timu tano ambazo ni Polisi Katavi, Makanyagio Fc, Kazima Fc, Majalila FC na Veta Mpanda.

Kundi B lina timu za Mpanda United, Mbugani FC, Faya FC na Baruti Kasokola ambapo kundi A litatoa washindi watatu kuingia hatua ya pili na kundi B litatoa timu mbili.

Katika Mchezo wa ufunguzi ulifanyika mchezo baina ya timu za polisi katavi na Makanyagio katika mchezo huo ambao ulihudhuliwa na mamia ya wakazi wa mji wa mpanda timu hizo zilitoka sale kwa kufungana goli moja kwa moja (1-1).

Mshindi wa kwanza wa mashiindano hayo atauwakilisha mkoa wa Katavi katika mashindano ya ligi ya Taifa ya mabingwa wa mikoa.