NDGE YA ZAN AIR YAANGUKA HUKO PEMBA

Abiria 17 akiwemo waziri wa katiba na sheria Zanzibar Mhe. Abubakari khamis bakar, na marubani wawili, wamesalimika kifo baada ya ndege ya shirika la ndege la 'Zanz air' kufeli breki, muda mfupi wakati ndege hio ilipo kuwa ikitua kwenye uwanja wa ndege wa Abeid amani karume, uliopo nje kidogo ya mji wa chakechake mkoa wa kusini Pemba.

Kwa mujibu wa tarifa zilizo tolewa na makamanda wa polisi mkoa kusini Pemba kamishina msaidizi swalehe mohamed swalehe na kamanda wa kikosi cha zima moto na uokozi pemba wamesema ndege hiyo wakati wa kutua ilipata hitilafu ya kufeli breki na kusereka hadi nje ya uwanja umbali wa mita mia mbili kwenye vichaka.

Wamesema abiria wote wametoka salama hakuna alie juruhiwa licha ya ndege hio kuacha uwanja kusereka kwenye nyasi na kungia kwenye mashamba ya muhogo kupita kwenye masiki majiti yalio katwa na kisha kusimama baada ya ringi kujizonga na mizizi ya pori hilo.

Ipo haja kwa mamlaka ya viwanja vya ndege nchini kutoa taaluma kwa watendaji wa kiwanja cha ndege kisiwani pemba kutoa ushirikiano kwa wandishi wa habari pale inapo tokea dharura kutokana na watendaji wa kiwanja cha ndege kisiwani hapa kushindwa kabisa kutoa ushirikiano kwa wandishi juu ya tukio hili.