Shuhuda Abdul Ally ambae ni mkuu wa nyumba zilizokaribu naalikopigwa Mwenyekiti huyu, anasema walisikia kelele za huyumtu kupigwa saa tisa usiku na walipomsogelea walimkuta peke yake.'Niliomba wasiniue, wamenipiga sana…
Wamenichukua saa tano nyumbani kwanguKwa Aziz Ally, wao walikua na gari kama ya Polisi lakini inaonekana sio ya polisi wakasema tunakupeleka Central, tulikua wanne na hawakuhangaika na mtu wakanichukua mimi moja kwa moja..
Tulipopanda kwenye gari wakachukua nguo yangu wakanifunga uso,wakaanza kunipiga wakisema nisiwajibu na hawakuniambia chochote.