Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewavua uanachama, aliyekuwa mjumbe wa kamati kuu Dr.Kitila Mkumbo na aliyekuwa Mwenyekiti Mkoa wa Arusha Samson Mwigamba kwa kosa la uhaini ndani ya chama.
Pia uongozi wa Chadema umewapiga marufuku wanachama wake kushiriki katika mikutano ya Zitto Kabwe, kwa madai ya kukiukakatiba ya Chama na kwenda mahakamani kuzuia vikao vya kamati kuu kutojadili ajenda zake.