WAJUMBE WAMGOMEA WARIOBA

Uwasilishwaji  wa rasimu ya katiba uliokuwa ufanywe na mwenyekiti wa tume ya mabadiliko ya katiba Mh jaji Joseph  Warioba  umeshindwa kufanyika baada  ya baadhi ya wajumbe ambao ni wanachama wa umoja wa katiba ya wananchi kusimama na kuanza kuzomea, kupiga makofi  na  kuzungumza bila ya utaratibu wa kipinga kuwasilishwa kwa rasimu hiyo kwa kile walichodai  kuwa  kanuni zimekiukwa.

Siyo kwamba ni sokoni bali ni wajumbe wa bunge maaalum la katiba ambao wanapinga kuwasilshwa kwa rasimu hiyo ambapo licha ya mwenyekiti wa bunge hilo Mh Samweli  Sitta kumtaka jaji Warioba  kuendelea haikuwezekana.

Baada ya  hali hiyo wabunge ambao wanaunga mkono kitendo kilichofanyika cha  kuzuia kuwasilishwa kwa rasimu hiyo ambapo wali kilaani vikali.

Aidha kwa upande wa wabunge ambao wanaunga  mkono kilichotokea bungeni wamesema mwenyekiti  ameanza kwa kukiuka kanuni kana kwamba wakati zinapitishwa hakuwepo na hivyo hawawezi kamwe  kukubali kuburuzwa.

Hata hivyo licha ya kusitishwa kwa bunge hilo wajumbe waliendelea kukaa ndani ya ukumbi huo  wakipiga soga hatua ambayo pia ilipelekea kutolewa kwa tangozo lingine la kuwataka watoke nje.