MWANAJESHI FEKI ATUPWA JELA MIAKA MITATU

MAHAKAMA ya Wilaya ya Bunda mkoani Mara, imemhukumu kifungo cha miaka mitatu jela mwanamume aliyejifanya askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na kufanya utapeli.

Bakari Saibo (32) mkazi wa Mwenge jijini Dar es Salaam, alihukumiwa na Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Bunda, Said Kasonso, baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani na upande wa mashitaka.

Awali, Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Masoud Mohamed, alidai kuwa mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo Februari 28 mwaka huu, saa 12:15 jioni.Alidai mshitakiwa huyo akiwa katika eneo la nyumba moja ya kulala wageni iitwayo Mori iliyoko mtaa wa Posta mjini Bunda, alijitambulisha kwamba ni askari wa JWTZ.

Aidha alidai mshitakiwa alijitambulisha kwa Kamira Nkengemkazi wa mtaa huo aliyemtilia shaka na kutoa taarifa Polisi. Alidaimbali na kujitambulisha hivyo, pia alimtapeli Nkenge nguo zake zenye thamani ya Sh 100,000 na kwamba baada ya polisi kupata taarifa hiyo, walimkamata na kumpeleka mahakamani hapo.

Hakimu Kasonso alisema kosa la kwanza la kujifanya mwanajeshi wa JWTZ, anamhukumu kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela na kosa la pili la utapeli anamhukumu kifungo cha miaka miwili jela.

Adhabu hizo zatazitumika kwa pamoja. Kabla ya hukumu kutolewa mwendesha mashitaka wa Polisi, aliiomba Mahakama hiyokutoa adhabu kali kwa mshitakiwa, kwani tabia hiyo inachafua sifa za majeshi.