AHUKUMIWA MIAKA 30 JELA KWA KULAWITI

Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imemuhukumu Wiliamu George 32 Mkazi wa Mtaa wa Nsemlwa Wilaya ya Mpanda kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti kijana mwenzie 22 Mkazi wa Mtaa wa Mpanda hoteli baada ya kumnywesha pombe ya kienyeji kupita kiasi.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu mkazi mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa na hukumu hiyo kuvuita hisia za watu mbalimbali wa maeneo ya mjiwa Mpanda na Mkoa wa Katavi.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu wa mahakama hiyo baada ya mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo wa upande wa mashitaka na upande wa utetezi Katika kesi hiyo hapo awali mwendesha mashita mkaguzi wa jeshi la polisi Ally Mbwijo alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo hapo Novemba 21 mwaka jana majira ya kumi na mbili jioni katika mtaa wa Mpanda Hotel.

Mshitakiwa siku hiyo ya tukiokabla ya kutenda kosa hilo la kumlawiti kijana huyo alidaiwa kunywesha pombe ya kienyeji aina ya komoni walikuwa wakichanganya na bia nyumbani kwa mwamke aliyekuwa akiwauzia pombe aliyetambulika kwa jina moja la Lita katika mtaa huo wa Mpanda hotel.

Ilielezwa na mwendesha mashita Ally Mbwijo kuwa mshitakiwa baada ya kuona mwenzake ametoka nje kwenda kujisaidia alimwagiza dukani Lita aende akamnulie sigara.

Aliileza mahakama baada ya kijana huyo ambae jina lake limehifadhiwa kurudi ndani aliendelea na kunywa pombe ambayo alikuwa imeisha kwenye chupa yake na ndipo alipoteza fahamu na mshitakiwa alitumia nafasi huyo kumwingilia kinyume cha maumbile yake huku akiwa amemlaza kwenye kochi.

Mwendesha mashitaka alieleza Lita alipotoka dukani alimkuta mshitakiwa akiwa amekaa karibu na kijana huyo ambae alikuwa amevuliwa nguo yake ya saruali na akiwa ajitambui na sehemu zake za matakoni zikiwa na mbegu za kiume.

Mshitakiwa baada ya kufanya kitendo hicho siku iliyofuata alimtuma mama yake mzazi aende kwa kijina huyo akamwombee samahani kwa kile alichoeleza kuwa anahofia kufungwa jela.

Baada ya mama mshitakiwa Wiliamu George kumwombea msamaha kwa kijana alilawitiwa alikubali kumsamehe mshitakiwa kwa kuhofia kupata aibu.

Mshitakiwa baada ya kusamehewa alianza kumtangaza kijana huyo kwa rafiki zake na kuwafahamisha kuwa kijana huyo ni shemeji yao kitendo ambacho kilimkasilisha kijana huyo na kuamua kwenda kituo cha polisi kutoa taarifa ya kulawitiwa kwake na Mshitakiwa Wiliamu George.

Hakimu mkazi mfawidhi Chiganga Ntengwa kabla ya kutowa hukumu hiyo aliiambia mahakama kuwa mahakama imemtia hatiani mshitakiwa Wiliamu George kwa kosa la kumwingilia kijana huyo kinyumbe na maumbile yake hivyo mahakama inatowa nafasi kwa mshitakiwa kama anasababu ya msingi ya kuishawisha mahakama impunguzie adhabu aieleza mahakama hiyo.

Katika uetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama imwachie huru kwani yeye hakutenda kosa hilo na pia umri wake bado ni kijana mdogo na wazazi wake bado wanamtegemea maombi ambayo yalipingwa vikari na mwendesha mashitaka.

Hakimu Chiganga baada ya kusikiliza utetezi huo aliiambia mahakama kuwa mshitakiwa amehukumiwa na mahakama baada ya kupatikana na hatiaya kumwingilia kinyume na maumbile kijana huyo na anahukumiwa na adhabu ya kifungu cha sheria namba 235 sura ya 20 ya mwaka 2009 hivyo Wiliamu George mahakama imehukumu kutumikia jela kuanzia jana kifungo cha miaka 30 jela.

Chanzo: Katavi yetu