JE ARSENAL KUWAONDOSHA THE BAVARIANS KWAO?

Michuano ya kuwania kombe la klabu bingwa barani Ulaya kuendelea leo usiku huku kukiwa na mechi mbili.

Arsenal, inaelekea, Bonn, kutoana jasho na mabingwa wa Ujerumani, Bayern Munich ambayo ilishinda mechi ya raundi ya kwanza kwa mabao mawili kwa nunge katika uga wa Emirates.

Hata hivyo Arsenal itakosa huduma za mcheza kiungo wake Kieran Gibbs ambaye kwa sasa anauguza jeraha la mkuu na mshambulizi Yaya Sanogo, lakini mlinda lango Laurent Koscielny, ambaye alikuwa akiuguza jeraha la paja anatarajiwa kurejea.

Kipa Lukasz Fabianski naye atachukuwa mahala pa Wojciech Szczesny, ambaye amesimamishwa kucheza kwa muda baada ya kupewa kadi nyekundu wakati wa mechi ya raundi ya kwanza.

Mwaka uliopita Arsenal iliishinda Bayern kwa magoli mawili kwa bila katika mechi ya marudiano lakini ilibanduliwa nje ya mashindano hayo baada ya kupoteza raundi ya kwanza 3-1.


Katika mechi nyingine ya marudiano leo usiku itakuwa kati ya Atletico Madrid na AC Milan.

Madrid ilishinda awamu ya kwanza kwa bao moja kwa bila.

Mario Balotelli huenda akajumuishwa kwenye kikosi cha wachezaji kumi na mmoja wa AC Millan, baada ya kuuguza jeraha la mgongo alilopata siku ya Jumamosi dhidi ya klabu ya Udinese.

Atletico nayo inamkaribisha mchezaji wake aliyefunga idadi kubwa yua magoli Diego Costa huku ikijaribu kufunzu kwa robo fainali ya kombe hilo kwa mara ya kwanza kwa zaidi ya miaka kumi na saba iliyopita.

Na ili kufuzu, mabingwa hao mara saba wa Ulaya ni sharti waandikishe historia ya kuwa timu ya tatu katika historia ya kombe hilo kuwahi kushindwa nyubani katika mechi ya raundi ya kwanza na ishinde mechi ya marudiano ugenini.


*BARCELONA KUIMALISHA MPIRA SOMALIA

Klabu ya soka ya Hispania Barcelona, imezindua mpango wakutoa mafunzo kwa makocha wa Somalia.

Mpango huo ujulikanao kama Futbal Net unalenga kuimarisha soka miongoni mwa vijana nchini Somalia, huku nchi hiyo ikijaribu kujiondoa kutoka katika vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Kamati ya michezo ya Olimpiki pia inaunga mkono mpango huo.Wanatumai kufungua vituo kadhaa vya mafunzo kote nchini humo.

Soka na michezo mingine ilikandamizwa na kundi la wanamgambo la Al Shabab kabla ya kuondolewa mjini Mogadishu miaka mitatu iliyopita.


*MASHABIKI KUTIZAMA MPIRA BURE

Mashabiki wa soka nchini Afrika Kusini watapata fursa ya kutizama mechi za ligi kuu ya England, katika bustani mpya itakayo funguliwa mjini Johannesburg mwisho wa mwezi huu.

Mechi tano, ikiwemo ile kati ya Arsenal na Manchester City itaonyesha moja kwa moja kwenye runinga kubwa katika bustani hiyo tarehe 29 na 30 mwezi huu.

Hafla hiyo ambayo haitatoza ada yoyote, inaandaliwa kwa mara ya kwanza na mashabiki elfu kumi na mbili wataruhusiwa kuingia ndani ya bustani hiyo ya Zoo LakeSports Club kila siku.

Mashabiki hao pia watapata fursa ya kukutana na wachezaji wa zamani wa timu ya taifa ya AfrikaKusini, Bafana Bafana akiwemo Mark Fish na Lucas Radebe.

Vile vile wachezaji wa zamani wa Liverpool, Robbie Fowler na mchezaji wa zamani wa Chelsea na nahodha wa Ufaransa Marcel Desailly watakuwepo.

Wakati wa hafla hiyo mashabiki watakuwa na fursa ya kuona na kupiga picha kombe la ligi kuu ya Premier ya England.