AFIKISHWA MAHAKAMANI KWA KUFUKUA KABURI

Mkazi wa kijiji cha Ikola Wilayaya Mpanda Mkoa wa Katavi Richard Clavery 34 amefikishwa Mahakamani katika mahakama ya Wilaya ya Mpanda kujibu tuhuma za kufanya vitendo vya ushirikina wa kufukua kaburi la mwanamke aliyekufa Mtuhumiwa alifikishwa kizimbani hapo Februari 25 mwaka huu mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakamaya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa na kusomewa mashitaka na mwendesha mashitaka Godfrey Luzabila.

Mwendesha mashitaka alidai Mahakamani hapo kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo hapo Februali 18 mwaka huu majira ya saa nne usiku nyumbani kwa Lenada Sakafu Mwendesha mashitaka Luzabila aliiambia mahakama kuwa siku hiyo ya tukio mtuhumiwa alifika nyumbani kwa Lenada Sakafu na kufukua maiti ya mdogo wake na Lenada aitwaye Tabu Omera ambae alikuwa amefarii siku tatu kabla ya tukio hili.

Aliendelea kuieleza Mahakama siku hiyo Lenanda alikuwa nyumbani kwake pamoja na majirani na ndugu zake wakiendelea kuomboleza msiba ghafla alitokea mtoto wake aitwaye Brandina na kuwaeleza kuwa ameona mtu nje akifukua kaburi la marehemu ambae alikuwa amezikiwa kwenye eneo la nyumba yao.

Alieleza ndipo watu hao walipoamua kutoka nje na kumkuta mtuhumiwa Richard Clavery akifukua kaburi hilo huku akiwa amevua nguo zake zote ambazo alikuwa amezitundika kwenye msalaba wa kaburi hilo na walipomsemesha mtuhumiwa alijifanya kupandisha majini.

Mtuhumiwa baada ya kusomewa mashitaka alikana na Hakimu Mkazi Mfawidhi Chiganga Ntengwa aliharisha kesi hiyo hadi hapo machi 6 na mtehumiwa alipelekwa lumande baada ya kushindwa kutimiza mashariti ya mdhamana ambapo alitakiwa adhaminiwe na mtu mmoja kwa dhamana ya shilingi milioni moja.

Chanzo: KATAVI YETU