JAJI MKUU: KUKIMBILIA MAHAKAMANI NI UPUMBAVU

Jaji mkuu wa Kenya Daktari Willy Mutunga amewakanganya wakenya baada ya kusema wanapaswa kuwatembelea waganga kutafuta suluhu ya matatizo yao badala ya kutegemea tu mahakama ya nchi hiyo.

Jaji Mutunga amewataka wakenya kutumia njia mbadala kama mazungumzo ili kutafuta suluhu wakati wa migogoro.

Jaji huyo amewashauri wakenya kutumia wazee wa vijiji, makanisa na miskiti kutatua migogoro na kusema kuwa yeye binafsi amewaambia watu wa jimbo la Kitui anakotoka kuwatembelea wachawi na waganga kutatua baadhi ya masuala yao.

Jaji mkuu aliyasema haya akiwa Gatundu katika eneo la kati alipokuwa akifungua mahakama mapya ya Kiambu.

Amesema kuwa huduma za mahakama ni ghali mno na akatoa wito kwa wanaotafuta haki mahakamani haswa kuhusu maswala ya familia, kutumia vikao vingine huku akiongeza kuwa mfumo wa kisheria

"Kusema tukutane kortini ni upumbavu mtupu kwa sababu pesa zenu zitaliwa na mawakili."

Afadhali muende kwa wazee au kwa viongozi wa kidini wa mahakama huchukua muda mrefu kuamua kesi na unaweza kusababisha mgawanyiko katika familia.

Amesema kuwa katiba, inaruhusu watu kutumia njia mbadala kutatua migogoro badala ya kutumia masaa mengi na kiasi kikubwa cha fedha kwa mawakili.

Kipengee cha 159 ya Katiba ya Kenya inawaruhusu wakenya kutafuta njia mbadala za kusuluhisha ubishi miongoni mwao.

Kesi zaidi ya 600,000 zipo kortini zikisubiri kuamuliwa na kulinganana jaji mkuu wa Kenya asilimia kubwa ya kesi hizi zinaweza suluhishwa nje ya mahakama.

Katika utamaduni wa Kiafrika ubishi mwingi ulikuwa unaamuliwa na wazee lakini maamuzi yao haswa katika maswala mengine kama vile ubakaji uhalifu na mauaji yakasababisha serikali kuingilia kati kwa kuwafikisha watuhumiwa mahakamani na hivyo ikapunguza hadhi ya vikao hivyo vya wazee miongoni mwa wakenya.

Katika sehemu nyingi nchini Kenya waganga na madaktari wa kienyeji huwa wanatumika kuwanasa wezi na washukiwa wa uhalifu.

Hata hivyo, kumetokea idadi kubwa ya watu wanaonadi huduma zao katika maeneo ya miji na kushukiwa kuwa ni walaghai tu kutokana na idadi kubwa ya magonjwa wanayodai kutibu ikiwemomagongwa ambayo hayana tiba kama vile Ukimwi.

Hoja yake tayari imezua mjadala mkubwa nchini Kenya ,Kiongozi wa Serikali bungeni Adan Duale, akimpuzilia mbali na kudai kuwa hiyo ni dalili kuwa ameshindwa na majukumu yake.

Idara ya mahakama nchini Kenya imelaumiwa kwa kushindwa kutoa uamuzi wa kesi haraka na kupelekea watu wengi kukata tamaa ya kupata suluhu baada ya kesi zao kutoamuliwa kwa zaidi yamiaka 5 hadi miaka kumi.