MTU MMOJA AFARIKI NA WENGINE 38 KUJERUHIWA

Mtu mmoja amefariki dunia na wengine 38 kujeruhiwa, kati yao 14 vibaya, baada ya magari matatu waliyokuwa wakisafiria, kugongana, mawili uso kwa uso, huku jingine likijaribu kukwepa ajali, katika eneo la Bwawani, barabara kuu ya Morogoro-Dar es saalam, wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

ITV imefika eneo la tukio na kushuhudia magari mawili kati ya yaliyohusika na ajali, yakiwa yameharibika vibaya, hasa sehemu ya dereva, ambapo mkuu wa usalama barabarani Chalinze mkoani Pwani, Inocent Sule, amesema chanzo cha ajali ni basi la abiria, mali ya kampuni ya Linowele class, lililokuwa likitokea dar es salaam kuelekea malinyi wilayani ulanga, , likiendeshwa na mtu aliyefahamika kwa jina moja la musa kujaribi kulipita gari jingine lililokuwa mbele na kukutana uso kwa uso na tenka la mafuta aina ya Iveco, ambapo dereva wa tenka, ali hassan ngoma, mkazi wa korogwe mkoani tanga, amefariki dunia papo hapo, huku yule wa basi hali yake ikiwa ni mbaya sana na la tatu mali ya kampuni ya adventure aina ya nisan diesel, lililokuwa likitokea Dar es salaam kuelekea Kigoma liliyagonga magari hayo yaliyokuwa yamepata ajali.

Mashuhuda wa ajali hiyo, wakiwemo majeruhi walionusurika kifo katika ajali hiyo, ambao baadhi yao wamekimbizwa kupatiwa huduma ya kwanza katika zahanati ya magereza bwawani, wamezungumzia kuhusiana na namna walivyobaini ajali hiyo, huku mganga wa zahanati ya sekondari ya magereza Bwawani, Lazaro Mdeka, akikiri kupokea majeruhi 38, na 14 hali zao ni mbaya na wamekimbiza hospitali ya rufaa ya mkoa wa morogoro kwa matibabu.

Katika hospitaliya mkoa wa Morogoro, huduma za kuwapokea na kuwahuduma majeruhi hao zimekutwa zikiendelea, huku wengi wakishindwa kuzungumza kutokana na hali mbaya.

Chanzo:ITV