DARAJA LA KIGAMBONI LAKAMILIKA KWA 45%

Daraja la Kigamboni limekamilika kwa zaidi ya asilimia arobaini na tano na matumaini makubwa ya kumalizika kwa ujenzi huo kwa muda uliopangwa Julai mwakani yakionekana huku nyumba zilizokuwa zinazuia ujenzi huko zikibomolewa kwa nguvu na serikali.

Akizungumza na ITV jijini Dar es Salaam meneja mradi huo injinia Karim Mattaka amesema ujenzi huo umeshaanza kuleta matumaini makubwa kutokana na nguzo mbili zilizokuwa zinakwamisha kuwa tayari na zoezi linaloendelea ni kuhamisha maji katika maeneo yalinayochimbiwa nguzo hizo sambamba na kuchimbia nguzo kubwa za kupokea baraja hilo upande wa barabara ya Mandela.

Aidha injinia Karimu amejaribu kufafanua mfumo wa barabara na daraja hilo namna utakavyotumika baada ya kukamilika na kuwahakikishia watanzania ujenzi huo utakamilika kwa wakata kama mambo yataenda kama yalivyopangwa.

Mwenyekiti serikali ya mtaa wa Vijibweni Bw. Athman Ally akielezea kuhusiana na hatua iliyochukuliwa na serikali ya kuvunja nyumba za baadhi ya wakazi waliogomea fidia amesema wao walipewa taarifa na mwanasheria mkuu na baadaye akatakiwa kwenda kusimamia zoezi la uvunjaji wa nyumba hizo.


Chanzo:ITV