UTURUKI YAIFUNGIA YOUTUBE

Serikali ya Uturuki imebana matumizi ya mtandao wa kijamii wa YouTube, siku moja baada ya mahakama kuamuru kusitishwa kwamuda marufuku ya Twitter ambayo waziri mkuu Recep Tayyip Erdogan alitangaza wiki jana.

Duru zinasema kuwa halmashauri ya usimamizi wa teknolojia ya mawasiliano nchini humo, imechukua hatua za kuudhibiti mtandao huo ingawa taarifa tofauti zinasema kuwa mazungumzo yanaendelea ikiwa hatua hiyo ichukuliwe.

Baadhi ya watumiaji wa mtandao huo walishindwa kuutumia kwani ulikuwa umebanwa wakati watu wenine katika sehemu mbali mbali walifanikiwa kuutumia.

Awali, kilichoonekana kama mawasiliano kati ya maafisa wa serikali hiyo wakizungumzia Syria yalifichuliwa kwenye mtandao huo wa kijamii.

Inaarifiwa mashauriano hayo yaligusia operesheni ya kijeshi dhidi ya Syria na yaliwashirikisha wakuu wa ujasusi , waziri wa mambo ya njena naibu mkuu wa jeshi.

Shirika la habari la Reuters linasema kuwa haliwezi kuthibitishakanda hiyo ingawa inaonekana kuwa taarifa muhimu sana ya serikali ya Uturuki kuwahi kufichuliwa.

Bwana Erdogan, atakayeshiriki uchaguzi mkuu siku ya Jumapili, anatuhumu mitandao ya kijami wa kueneza taarifa zisizo kweli, na alitishia kupiga marufuku YouTube na Facebook.