CHAMA CHA ALLIANCE FOR CHANGE AND TRANSPARENCY(ACT) CHATAMBULISHWA

KILE kinachotafsiliwa kuwa Demokrasia nchini imeanza kukuwa kutokana na wingi wa vyama vya kisiasa nchini vinaanzishwa, hivi leo chama kipya cha kisiasa nchini kimeanzishwa chama hicho kinajulika kama ACT,(Alliance for change And Transparency)maana yake ni Umoja wa Mabadiliko na Uwazi.

Hayo, yamethibitishwa leo Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Chama hicho kipya, Limbu Lucas Kadawi Wakati akitambulisha Chama hicho kwenye Mkutano na Waandishi wa Habari, ambapo alisema wamefikia maamuzi ya kuanzishwa chama hicho kutokana na Malengo mahususi ya kuwaleta watu pamoja.

"Tumeanzisha chama hichi cha kisiasa kwa malengoma hususi ya kuwaleta watu pamoja watanzania wanaoamini kwamba nguvu ya Pamoja inaitajika katika kuleta mabadiliko ya kweli ya kisiasa katika nchi hii, na kwamba uwazi na uadilifu ni tunu ambazo taifa hili linaitajika kwa sasa na Baadaye"alisema Limbu

Limbu alisema chama hicho cha ACT kinatakuwa kinaongozwa na misingi mikuu mitano ambayo ndio itakuwa nembo ya chama hicho.

"ACT tutakuwa na inaongozwa na misingi mikuu mitano ambayo ni Uzalendo,Usawa,Uadilifu Uwazi na uwajibikaji pamoja na Demokrasia ya Kweli" Alizidi kuongezea Limbu.

Limbu ikumbukwe Mwaka 2010 alikuwa Mwanachama wa cha Wananchi CUF na aligombania Ubunge kupitia Chama hicho kwenye Jimbo la Temeke na Alibwagwa kwenye uchaguzi huo na Mbunge wa CCM kupitia Temeke, Mr Mtevu na Baada ya Hapo na kwenda kuanzishwa chama cha ADC kabla ya kuanzishwa chama hichi.

Aliwataka wananchi wakiamini chama hicho kuwa ni Chama kitakachowaletea maendeleo.

Kwa upande wake Katibu mkuu Taifa wa Chama hicho Samsoni Mwigamba alisema Chama hicho kwa sasa kimeanda mipango mikubwa ya kuhakikishwa kinashinda kwenye Chaguzi Mbalimbali Zinazokuja.

"Kwa sasa ACT Tanzania imekwisha Kukamilisha Rasimu ya awali ya Katiba ambaye iliwezesha kupata usajili wa Muda na Zoezi la kuandikishwa wananchama katika mikoa kwa ajali ya kuomba usajili wa kudumu kwa mujibu wa sheria limekwisha kamilika"

"Tumewapata Wanachama katika mikoa yote ya Tanzania Bara,hata ivyo tumechagua mikoa kumi ambayo tungependa Msajili akahakiki kama sheria inavyotaka"alisema Mwigamaba.

Ikumbukwe Samsoni Mwigamba kabla ya kujiunga na chama hichi cha ACT alikuwa mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Mkoani Arusha na pia alikuwa mhasibu Mkuu wa Chama hicho na Baada ya hapo Chama chake cha Chadema kilimvua uwanachama kwa kile chama hicho kinadai kuwa Mwigamba alikuwa anafanya Uasi katika chama hicho, ambapo Kamati kuu ilimvua uwanachama pamoja na Wananchama wengine akiwemo Ziito Kabwe pamoja na Dk Kitara Mkumbo.

Wachambuzi wa Masuala ya Kisiasa waliozungumza na Mwandishi wa Mtandao huu walisema chama hicho kipya cha kisiasa nchini uwenda kikawa kimeanzishwa kwa mahususi ya kuwachukua wanachama waliokuwa wamevuliwa uwanachama kwenye vyama tofauti vya kisiasa nchini, huku wachambuzi hao wakihoji kwanini chama hicho cha kisiasa kimeanzishwa sasa, wakati vyama vya kisiasa nchini vikiwa katika hali ya sitofamu.

Ambapo Kauli hiyo ilipingwa vikali na Mwenyekiti wa Chama hicho cha ACT alisema chama hicho wala hakina uhusiano wowote na Mtu wala mikoa bali chama hicho kinawahusishwa watanzania wote.