JUHUDI ZA KERRY ZAGONGA MWAMBA

Juhudi za marekani kuwakutanisha kwa mara ya kwanza ana kwa na mawaziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Urusi na Ukraine kuhusu mzozo unaoendelea katika jimbo la Crimea zimegonga mwamba.

Ingawa waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Marekani John Kerry amekanusha kwamba palikuwa na nia ya kumkutanisha mwenzake wa Urusi Sergey Lavrov na waziri mpya wa mashauri ya nchi za wa Ukraine Andrii Deschchytsia iwapo wawili hao wangekutana mjini Paris ingekuwa ni mafanikio makubwa ya kidiplomasia.

Sergei Lavrov alikataa kukutana na waziri huyo mpya wa Ukraine kwa sababu Urusi haitambui utawala mpya wa mjini Kiev.

Akizungumza mjini Paris Bwana Deschchytsia amesema licha ya vuta nikuvute hiyo anaamini kwamba kuna dalili ya mafanikio katika mashauri." Kwa hiyo baada ya kuwa hapa siku nzima mjini Paris, inaonekana kwamba tunaendeleana mashauri yetu na tunaamini kwamba tutapata mwafaka.

Ninaelekea mjini Brussels kukutana na waziri mkuu kujadili hatua zaidi za kuchukua. Shukran.

"Na alipoulizwa na mmoja waandishi wa habari ni kwa nini hakuweza kukutana na waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Urusi Sergey Lavrov hivi leo, bwana Deschchytsia alijibu- ''kamuulize Lavrov mwenyewe.''

Hata hivyo bwana Lavrov alifanya mazungumzo ya kina na waziri wamashauri ya nchi za kigeni wa Marekani John Kerry na mawaziri wengine wa umoja wa ulaya. Bwana Kerry alitaja mkutano huokuwa mgumu lakini akasema ana ujumbe atakaoupeleka kwa rais Obama na mazungumzo yataendelea.

Waziri wa mashauri ya nchini za kigeni wa Ufaransa Laurent Fabius kadhalika alielezea matumaini ya mazungumzo hayo kufanikiwa."

Tumekubaliana kuendelea na mashauri kwa sababu mambo bado na hali sio rahisi anasema bwana Fabius. Lakini tunayo furaha kwamba siku ya leo mjini Paris imeturuhusu kuanzisha mikakati.''

Kwa upande mwingine rais wa Urusi Vladmir Putin alifanya mazungumzo kuhusu mzozo huo na chanzela wa Ujerumani Angela Merkel kwa njia ya simu.

Wakati huo huo Mwakilishi mkuu wa Umoja wa mataifa huko Crimea, Robert Serry, amelazimika kukatiza ujumbe wake baada ya kutishiwa na watu waliojihami alipokuwa akitoka katika makao makuu ya jeshi la wanamaji la Ukraine katika bandari ya Simferopol.