LIBYA YAOMBA MSAADA UN

Libya inaiomba jumuiya ya kimataifa kuisaidia kupambana na kile inachosema ni vita dhidi ya ugaidi.

Katika taarifa iliyosambazwa Jumatano jioni serikali ya muda nchini humo ilisema inaomba hususa ni msaada wa Umoja wa Mataifa katika kutokomeza ugaidi kutoka miji ya Libya. Ilisema makundi ya ugaidi yanaendesha operesheni zake huko Benghazi, Sirte na maeneo mengine.

Benghazi ilikuwa eneo lililotegwa bomu ndani ya gari siku ya Jumatatu tukio ambalo liliuwa watu wasio pungua saba.

Serikali imekuwa ikipambana na vitisho vya usalama tangu kuondolewa kwa Moammar Gadhafi mwaka 2011. Makundi mbali mbali ya wanamgambo ambayo yalisaidia kuondolewa kwa kiongozi wa muda mrefu nchini humo yanaendelea kuendesha operesheni zao kwenye maeneo makubwa ya Libya ikiwemo huko mashariki mwa Libya ambako wamechukua udhibiti wa maeneo makubwa.

Viongozi wa muda wameyaagiza majeshi maalumu nchini Libya kukamata tena bandari katika wiki kadhaa zijazo.

Jumatatu kikosi maalumu cha Marekani cha NAVY SEAL kilichukua udhibiti wa lori moja la mafuta ambalo lilijaza mafuta ghafi kutoka bandari inayoshikiliwa na waasi ya As-Sidra kabla ya kuvamia majeshi ya Libya kwenye eneo lakuingia maji ya kimataifa karibu na Cyprus.

Libya inasema waasi hawawezi kuuza kihalali mafuta nchini humo lakini kupoteza udhibiti wa bandari huko mashariki kumezorotesha serikali kuwa na uwezo wake wenyewe wa kuuza mafuta na kusababisha usafirishaji wa nje kushuka kwa asilimia 80.

Umoja wa Mataifa ulijibu juu ya hali hiyo hapo Jumatano kwa azimio la Baraza la Usalama kupiga marufuku uuzaji usio halali wa mafuta ghafi kutoka Libya.