AVB AIBUKIA URUSI HUKO ST. PETERSBURG

Aliyekua Kocha wa Tottenham na Chelsea, Andre Villas-Boas ameridhia kuingia mkataba wa miaka miwili na klabu ya Zenit St Petersburg, taarifa za klabu hiyo ya Urusi zimeeleza.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 36, aliyetimuliwa na Spurs mwezi Desemba atachukua nafasiya Luciano Spalletti.

Villas-Boas atatangazwa rasmi kuwa Kocha mkuu wa Timu hiyo tarehe 20 mwezi Machi.

Kibarua cha Spalletti kiliota nyasi baada ya Spurs kupoteza mchezo wa kwanza hatua ya 16 bora ambapo ilipigwa mabao 4-2 na Borussia Dortmund.

Villas-Boas alikuwa sehemu ya kikosi cha uongozi cha Jose Mourinho kabla ya kujiunga na Academica na Porto za nchini kwake Portugal.

Aliwezesha ushindi wa kombe la ligi, ligi ya Europa katika msimu wake wa kwanza akiwa na Porto kabla ya kujiunga na Chelsie mwaka 2011, lakini alitemwa na timu hiyo mwezi March mwaka 2012 baada ya kushindwa kuifikisha timu hiyo kwenye viwango bora.