URUSI YAITAMBUA CRIMEA KAMA NCHI HURU

Rais wa Urusi Vladmir Putin ametia saini ilani ya katiba inayotambua jimbo la Crimea kama taifa huru. Hatua hiyo inajiri muda mfupi baada ya marekani na Muungano wa Ulaya kutangaza vikwazo dhidi ya maafisa wa serikali ya Urusi na wa Ukraine waliohusika na njamaya Moscow kuiondoa Crimea katika Ukraine.

Rais Obama amesema kuwa anataka kuweka bayana kwamba kutakuwa na adhabu kwa wale walioanzisha mikakati ya Crimea kujitenga na Ukraine akiongeza kuwa vikwazo zaidi vitatolewa. Hata hivyo amesisitiza kuwa badokuna njia ya kusuluhisha mzozo huo kwa njia ya kidiplomasia.

Awali bunge la Crimea lilitangaza rasmi kuwa jimbo hilo liko huru kutoka kwa Ukraine na kutoa maombi ya kujiunga na mataifa yanayobuni muungano wa Urusi.

Balozi wa Marekani nchini Ukraine, Geoffrey Pyatt, ameiambia BBC kwamba ilani iliyotiwa saini na rais Putin kutambua uhuru wa Crimea haitabadili mtizamo wa Marekanikuhusu hali ilivyo." Kadri marekani inavyozingatia, hapatakuwa na mabadiliko kuhusiana na makadirio yetu kuhusu hali, mtizamo wetu wa Crimea kama sehemu ya Ukraineiliyo huru na mtizamo wetu kuhusu kwamba kura ya maamuziya siku ya jumapili iliyofanyika baada ya uvamizi wa kijeshi uliotekelezwa na Urusi ni kinyume na sheria kwa vyovyote," anasema.

Msemaji wa Ikulu ya White House Jay Carney, alipoulizwa na waandishi wa habari ikiwa rais Putin atalengwa baadaye na vikwazo hivyo amesema kuwa Marekani haitawasaza baadhi ya watu katika uwezekano wa kuwawekea vikwazo."

Uwezo wa kutoa vikwazo dhidi ya watu mbali mbali upo. Tutatoa tathmini kuhusu hatua mwafaka wakati hali ikiendelea kubadilika.

Hatutawasaza baadhi ya watu. Kutakuwa na gharama kwa Urusi, Gharama ya ziada itakayotolewa kwa Urusi, ikiwa Urusi hatabadili mwelekeo hapa kuhusiana na jinsi inavyoshughulikia hali nchini Ukraine," anasema.

Miongoni mwa maafisa waliolengwa na vikwazo vya Marekani na Muungano wa Ulaya ni maafisa wa ngazi ya juu katika utawala wa jimbo la crimea, rais wa Ukraine aliyengolewa madarakani Viktor Yanukovich, naibu waziri mkuu wa Urusi, wabunge wa Urusi na makamanda wa jeshi.