WACHINA MIAKA MITANO JELA AU FAINI YA MILIONI MOJA

RAIA wawili wa China wamehukumiwa kifungo cha miakamitano jela au kulipa faini ya Sh milioni moja baada ya kukutwa wakisafirisha meno ya tembo.

Qui Wu (30) na Zou Zhihong (51) ambao walikutwa na meno ya tembo, zilizotengenezwa kama bangili na kinyago.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Janeth Kinyage alisema washitakiwa watatumikia kifungo cha miaka mitano au kulipa faini.

Zhihong aliomba mahakama impunguzie adhabu, kwa kuwa ana matatizo ya moyo na ana familia inamtegemea na mama yake ni mzee.

Mwendesha Mashitaka Nassoro Katuga alidai Februari 23 mwaka huu eneo la Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) Wilaya ya Ilala, raia hao wa China walikutwa na vipande nane vya bangili, vilivyotengenezwa kwa meno ya tembo vyenye thamani ya Sh 249,600.

Pia, mshitakiwa Zhihong alikutwa na bangili mbili na kinyago, vilivyotengenezwa kwa meno ya tembo yenye kilogramu 0.25 yenye thamani ya Sh 240,000.