OSCAR PISTORIUS AKANA MASHITAKA

Mwanariadha wa Afrika Kusini Oscar Pistorius amekanusha mashitaka ya kumuua mpenzi wake wakati kesi yake ikianza kusikilizwa mjini Pretoria.

Pistorius ambaye ana ulemavu wa miguu na ambaye hutumia miguu bandia ameshitakiwa kwa kumuua mpenzi wake na mwanamitindo Reeva Steenkamp.

Oscar amesema alimpiga risasi marehemu kimakosa kwani alidhani alikua mwizi.

Katika siku ya kwanza ya kesi hiyo jirani wa Oscar Michelle Burger , ameambia mahakama kuwa alisikia mwanamke akipiga mayowe mapema asubuhi tarehe14 mwezi Februari mwaka 2013.

Bwana Pistorius amekanusha madai dhidi yake kuwa alimuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.

Alimpiga risasi na kumuua Steenkampe aliyekuwa na umri wa miaka 29 mwanamitindo na muigizaji akisema kuwa hakumuua kwa maksudi.

Jirani ya Oscar alisema kuwa kiliocha mwanamke huyo kilifuatiwa na milio ya risasi ''alipiga nduru akitaka msaada. Pia alisikia mwanamume akipiga mayowe naye akiomba msaada, ''alisema mwanamke huyo.

Alisema punde alipopiga simu kutaka msaada kutoka kwa polisi hapo ndipo alisikia milio ya risasi.

Kukamatwa kwa Pistorius kulishangaza wengi nchini Afrika Kusini.

Pistorius mwenye umri wa miaka 27 alishinda dhahabu katika michezo ya Olimpiki ya walemavu mjini London mwaka 2012 na pia alishindana katoka michezo rasmi ya olimpiki.

Kesi hiyo ilicheleweshwa wa dakika 90 kwani mkalimani wa lugha ya Afrikaans hakuwepo mahakamani.

Pistorius inasemekana alionekana mtulivu alipowasili mahakamani.

Pistorius anasema kuwa alimpiga risasi Reeva kwa bahati mbaya akidhani alikuwa jambazi aliyekuwa amevamia nyumba yake. Mauaji yake yalitokea siku ya Valentines mwaka jana.

Wiki jana mashirika ya habari za michezo, yalipata idhini ya kupeperusha kesi ya Pistorius moja kwa moja kutoka mahakamani.