POLISI WAKAMATA SHABA ZILIZOPORWA

Jeshi la polisi kwa kushirikiana na polisi wa kimataifa -interpol kanda ya Afrika limefanikiwa kuokoa kwa kuikamata katika kontena shaba yenye thamani ya zaidi ya dola 320,000 sawa na shilingi za kitanzania milioni 500 mali ya mfanyabiashara Fahmy Bin Kleb iliyokuwa imeporwa Februari mwaka huu eneo la mikumi mkoani Morogoro.

Akielezea tukio hilo mmoja wa wenye mzigo huo uliopatikana bwana Salmin Bin Kleb amebainisha kuwa kutokana na upelelezi waliofanya wamegundua kuwa baada ya mzigo huo kuporwa, watekaji wamepitisha mzigo huo maeneo mbalimbali kwa njia za magendo ukiuzwa na watu mbalimbali ikiwemo nchini Kenya na ulikuwa njiani kupelekwa Taiwan kabla ya kuwekewa mtego na kukamatwa katika meli yenye namba 1014 Hermes arrow safmarine ilipopitishwa nchini kuongezea mzigo.

Bwana Kleb pamoja na kupongeza na kushukuru kwa jitihada zilizofanywa na jeshi la polisi ambao wamesha wakamata watu kadhaa kuhusiana na tukio hilo, wizara ya mambo ya nje kupitia balozi wa Tanzania nchini Kenya balozi Batilda Buriani na waziri wa uchukuzi ameomba sheria ifuatwe bila uwepo wa urasimu ili haki itendekea kwa wakati.