AL SHABAAB WASHAMBULIA AMISOM

Kundi la wanamgambo la Al Shabaab nchini Somalia, linasemakuwa limeshambulia msafara wa magari ya kikosi cha Muungano wa Afrika, AMISOM, karibu na mji mkuu Mogadishu.

Walioshuhudia shambulizi hilo wanasema kuwa walisikia milipuko mikubwa katika eneo la Alamada lililo umbali wa kilomita20 kusini mwa mji mkuu.

Shambulizi lilitokea wakati magari ya kikosi hicho yalipolipukiwa na mabomu yaliyokuwa yametegwa ndani ya gari.

Al Shabaab wamasema kuwa wanajeshi saba wa AU waliuawa lakini AMISOM imesema kuwa hapakuwa na majeruhi wowote.

Kikosi hicho kilisema kuwa kilimpiga risasi dereva wa gari hilo alipokuwa anawakaribia ana hivyo kutibua shambulizi hilo.