PICHA ZA SATELITE ZA MABAKI YA MH370

Serikali ya Malaysia imesema kuwa picha mpya za Satelite zimeonyeshazaidi ya vifaa miamoja vinavyodhaniwa kuwa mabaki ya ndege yake iliyotoweka zaidi ya wiki mbili zilizopita.

Waziri wa usafiri wa nchi hiyo, Hishammuddin Hussein, amesema kuwa picha hizo zilizotolewa na Ufaransa, zinaonyesha vifaa hivyo kuwa zaidi ya mita ishirini kwa urefu.

Hadi kufikia sasa, hakuna taarifa rasmi ya mabaki ya ndege hiyo kuonekana.

Ndege hiyo iliyokuwa na abiria 239, ilikuwa safarini kutoka Kuala Lumpur kuelekea Beijing zaidi ya wiki mbili zilizopita.

Msako uliofanywa baharini na angani, kuitafuta ndege hiyo umeanza tena katika pwani ya Australia baada mawimbi kutulia baharini.