BAN KI MOON ATUA URUSI

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban ki Moon anatarajiwa kufanya mazungumzo leo na rais wa Urusi Vladimir Putin mjini Moscow katika juhudi za kutafuta suluhu ya kidiplomasia kuhusu Crimea.

Mkutano huo unafuatia majibizano makali baina ya mabalozi wa Marekani na Urusi katika Umoja wa Mataifa katika kikao cha baraza la usalama la Umoja huo New York.

Balozi wa Urusi Vitaly Churkin alisema watu wa Crimea walitekeleza haki yao kuhusu malengo yao.

Akijibu hoja hiyo balozi wa Marekani Samantha Power alisema kile kinachoitwa kura ya maoni ilikuwa ni maigizo na maelezo ya bwana Churkin yanaonyesha tu ndoto za ubabe wa Urusi.

Churkin alitishia kuwa Urusi inaweza kujiondoa katika masuala mengine ya ushirikiano.

Ziara ya Bwana Ban inafanyika wakati mkutano wa siku mbili wa Muungano wa ulaya ukianza mjini Brussels ambapo viongozi watafanya mazungumzo magumujuu ya uwezekano wa kuweka vikwazo zaidi dhidi ya Urusi.