WAANDAMANA DHIDI YA UN

Zaidi wa raia elfu moja wa Sudan Kusini, wameandamana katika mji mkuu wa nchi hiyo Juba, dhidi ya Umoja wa Mataifa, wakiishutumu kwa kuwapa waasi wanaopambana na serikali silaha.

Waandamanaji hai wamemtaka mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa nchini humo Hilda Johnson kujiuzulu.

Siku ya Ijumaa, serikali ya Sudan Kusini, ilisema kuwa ilinasa msafara wa magari yaliyokuwa yakisafirisha silaha ambazo huku zikidai kuwa zilikuwa zikisafirisha misaada ya chakula.

Umoja wa Mataifa umekanusha shutuma hizo, lakini imekiri kuwa imekiuka mkataba waliosaini na serikali ya nchi hiyo, kwa kusafirisha silaha wakitumia magari badala ya ndege.

Taifa la Sudan Kusini, limekumbwa na mzozo wa kisiasa tangu Desemba mwaka uliopita, wakati wanajeshi watiifu kwa makamu wa rais wa zamani wa nchi hiyo Riek Machar, kuanzisha mapigano katika kambi kuu ya jeshi mjini Juba.

Mazungumzo ya amani kati ya wawakilishi wa serikali ya Sudan Kusini inayoongozwa na Salva Kirrna makamu wake wa zamani RiekMachar, yanaendelea mjini Addis Ababa, Ethiopia.