MARUFUKU KUTEMBEA KIFUA WAZI KATIKA BUSTANI UINGEREZA

Wanaume wanaovua mashati wamepigwa marufuku kuitembelea bustani ya mapumziko na kujivinjari ya Adventure Island.

Ni eneo ambalo watu wanakwenda kujivinjari na familia zao, kwa kutazama wanyama, watoto hupata kubembea na pia watu huota jua.

Bustani hiyo iliyopo mjini Southend nchini Uingereza, imeweka ilani zinazowaomba wanaume wasivue mashati yao, na kwamba watakao patikana watafukuzwa.

Mkurugenzi mkuu, Marc Miller, amesema anataka wanaume waonyeshe "ustaarabu".

Bustani hiyo inasifika duniani kwakuwa na idadi kubwa ya watu walio uchi walioipanda bembea ya 'Rollercoaster' - licha ya kwamba ni jambo linalofanyika faraghani.

'Kuilenga Familia'

Zaidi ya watu 100 walivua nguo ilikuipanda bembea hiyo ijulikanayo kama Green Scream mnamo 2010.

Miller anasema: "Katika miaka yahivi karibuni, tumekuwa tukiongeza idadi ya vijana na wanaume ambao huvua mashati yao ili kupata joto la jua kwa wingi. Hilo ni sawa kabisa lakini katika mazingira yanayofaa".

"Tunajaribu sana kufanya biashara inayoivutia familia na sio kila mtu anavutiwa kuona vifua wazi".

Pamoja na kuwa na idadi kubwa duniani ya watu wasio vaa nguo, Adventure Island pia ilijaribu kuweka rekodi mpya ya kuwa na watu wengi wanaocheza mpira wagofu wakiwa uchi, mnamo mwaka 2012.

Msemaji mmoja anasema michezo yote hufanyika faraghani.

"Wanaohudhuria michezo hiyo ni waliojisajili kushiriki, ili kuchanga fedha nyingi za misaada ya kukabiliana na magonjwa kama saratani ya matiti na ya uume," alisema.

"Marufuku hiyo imetolewa wakatibustani imefunguliwa kwa umma."